Monday 15 April 2013

TIMBWILI : MUME wa mtu nusura auawe na KIMADA

WAKATI Oparesheni Fichua Maovu katika jamii inayoendeshwa na Global Publishers ikiwa kazini, wikiendi iliyopita ilinasa timbwili ‘hevi’ la aina yake kwa mwaka 2013 ambapo mume wa mtu, Joseph Hussein (31), nusura auawe na kimada, Ijumaa Wikienda linakumegea sinema ya bure. Tukio hilo lililokusanya umati lilijiri maeneo ya Mwenge, Dar mishale ya saa 10 usiku ambapo mwanaume huyo, mkazi wa Tegeta, alikiri kupokea kipigo almanusra apoteze uhai kutoka kwa mwanamke huyo aliyetambuliwa kwa jina Neema Samson, mkazi wa Buguruni.Habari za uhakika ni kwamba Neema alidai kuwa mwanaume huyo ambaye ni mume wa mtu ana tabia ya kumtafuta yeye kwa ajili ya huduma ya mapenzi lakini akishakidhi matakwa yake huwa hataki kutoa fedha kama wanavyokubaliana.
TUJIUNGE ENEO LA TUKIO
Fichua Maovu ikiwa mzigoni kunasa matukio machafu katika jamii likiwemo lile sugu la usaliti kwa wanandoa, ilipofika eneo la tukio, ilisikika sauti ikitokea gizani ikiita, mwizi…mwizi…mwizi…Timu ya Ijumaa Wikienda ilitii sauti hiyo na kuelekea kule ilikokuwa ikitokea ambapo Neema alikuwa amemkwida shingoni Joseph huku akilalamika kuwa anataka ujira wake.


SEKESEKE LAFUNGA MTAA
Kutokana na sekeseke hilo la kupigana, watu kibao walitoka nje ya nyumba zao na kushuhudia kilichotokea ambapo walipigwa na butwaa huku wakilalamika kuwa waliamshwa usingizini na watu waliokuwa kwenye starehe zao.


WAAMKA NA BOKSA, NIGHTDRESS
Huku wakiwa na boksa, night dress, vipensi na wengine mataulo, majirani wa eneo hilo walimshuhudia Neema akiwa amemkaba Joseph shingoni hadi akashindwa kupumua na kusababisha hekaheka mtaa mzima.“Kha! Mwanamke amemkaba mwanaume anataka kumuua kisa ni nini?” alihoji mmoja wa majirani hao.


Neema alikuwa akimnyonga Joseph kwa kutumia fulana yake akilalama kuwa amezoea kupewa penzi kisha kuingia mitini bila kulipa.“Namjua ni mume wa mtu, ni kweli nimefanya naye mapenzi na kama hamuamini niwaoneshe (huku akipandisha nguo na kubaki mtupu), nataka buku kumi na tano yangu la sivyo namtoa roho,” alisikika Neema akifoka kwa hasira.Wakiwa eneo la tukio, mjumbe wa nyumba kumi alifika na kuwashuhudia wakigaragazana mchangani ambapo Joseph alidai kuwa Neema alimwibia simu yake aina ya Nokia.

MJUMBE ATEMA CHECHE
Kwa upande wake, mjumbe wa nyumba kumi alijitahidi kwa uwezo wake wote kuwaamua lakini ilishindikana kwani Neema aliendelea kumkwida Joseph akidai ujira wake kwani tayari simu aliyokuwa ameisunda kwenye nyeti, alikuwa ameshanyang’anywa na wasamaria wema.

SOO HILOOO POLISI
Wawili hao waliendelea kuvutana hadi wasamaria wema waliposhirikiana kuwabeba kisha kuwapakiza kwenye Bajaj na kuwapeleleka kituo cha polisi....
Picha zaidi za tukio angalia hapa chini















Kwa habari zaidi soma gazeti la : BOFYA HAPA

0 maoni: