Monday 15 April 2013

Mwanamke anusurika kuuawa na PADRI amabye ni mpenzi wake huko kibaha

Bi Celestina Ananius(35) amenusurika Kuuawa na Padri   wa kanisa katoliki parokia ya hombolo iliyoko dodoma kwa jina la celestine john nyaumbana  ambaye kwa Sasa anaishi kwenye Makazi ya Katoliki Mbezi kwa ajili ya Masomo. Dada huyo anasema amekuwa katika mapenzi  na padri huyo tangia akiwa Fratel,akawa Shemasi na sasa ni padri nasuala hilo ni siri yao na wazazi wa pande mbili hadi wamezaa mtoto anaitwa Agnes(3).
Bi Celestina ambaye anaishi Dodoma alikuja Dar kumfuata Mpenzi wake huyo ili  ajue  hatima  ya  huyo  mtoto  wao....

Sasa wakati wapo dar padri huyo alimuomba mpenzi wake huyo watoke kidogo kwenda kutembea maeneo ya kiluvya...

Walipofika  huko wakati wapo katikati ya poli padri huyo alishuka kwenye gali na kumshambulia dada huyo  kwa madhumuni ya kumuua na kupoteza ushaidi ila hakufanikiwa kumuua .....

Taarifa za Polisi Mkoa wa Pwani zinaonyesha kuwa Mwanamke huyo aliokolewa na Wasamalia wema na kukimbizwa Hospitali ya Tumbi Kibaha kwa matibabu!!!

Kwa hisani ya - Mpekuzi

0 maoni: