Saturday 18 January 2014

Mwanamke mjamzito anaswa akifanya ukahaba!

OPARESHENI ya Polisi wa Mkoa wa Morogoro na kikosi maalum cha kufichua Maovu cha Magazeti ya Global Publishers (OFM), imemnasa mwanamke mjamzito katika kamatakamata ya machangudoa. Katika oparesheni hiyo ya aina yake iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Msamvu (Kambi ya Itigi), wanawake 30 waliodaiwa kujihusisha na biashara hiyo walikamatwa.

Waandishi wetu wakiwa na askari wa mkoa huo walimnasa mjamzito huyo anayedaiwa kuwa na mimba ya miezi sita akiwa mawindoni eneo hilo.
Mara baada ya mjazito huyo kukamatwa alitoa yake ya moyoni kwa kusema kwamba anafanya biashara hiyo ili kupata fedha za kujikimu na ujauzito wake haumpi shida yoyote.
“Jamani natafuta pesa za kujikimu na maisha hapa mjini sasa mnatukamata tukale wapi? Hii mimba ni yangu na ninayefanya ukahaba ni mimi niacheni,” alisema mdada huyo.
Pamoja na maneno yake, polisi walimbeba msobemsobe na kumfikisha kituoni pamoja na makahaba wengine.

Kwa hisani ya GPL

0 maoni: