Tuesday, 10 December 2013

Mwanamke aliyedai kubakwa ahukumiwa Somalia

Mahakama nchini Somalia, imemhukumu kifungo cha nyumbani mwanamke aliyedai kubakwa pamoja na waandishi wawili wa habari waliomhoji kuhusiana na madai hayo. Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 19, alipewa kifungo cha nje cha miezi sita kwa kile mahakama ilisema ni kutoa taarifa zisizokweli.
Atalazimika kukaa nyumbani kwake bila kutoka nje kwa miezi sita. Mmoja wa waandishi wa habari, aliyemhoji mwanamke huyo naye alipewa kifungo cha nje cha mwaka mmoja huku mwenzake akipokea kifungo cha miezi sita.
Waandishi hao wanafanya kazi na kituo cha redio Shabelle ambacho serikali ilifunga matangazo yake mwezi Oktoba baada ya polisi kuvamia ofisi zake.

Kwa hisani ya BBC Swahili

Related Posts:

  • Ukatili uliopitiliza ....Ndugu wataka MTOTO auawe MTOTO aitwaye Mwajuma Haji (16) ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili anayesumbuliwa na  ugonjwa wa kusinyaa kwa viungo yuko katika hali mbaya baada ya baadhi ya ndugu kudaiwa kutaka auawe ili kutoa u… Read More
  • Watu wavamia Kanisa na kuua Mtu mmoja ameuawa na wengine watatu kujeruhiwa kufuatia shambulizi lililofanywa na kundi la watu wasiofahamika usiku wa kuamkia leo katika kanisa la Gilgal Christian Worship Centre lililopo eneo la Pasiansi wilaya ya Ileme… Read More
  • Mfanyakazi wa ndani anyonga mtoto! NI ukatili uliopitiliza! Hausigeli aliyejulikana kwa jina moja la Ester (14) yupo matatani kwa madai ya kumuua mtoto Arafat Allan (3) kwa kumnyonga shingo na kumpiga na kitu kizito kichwani kisha kuutumbukiza mwili wake kw… Read More
  • Mama wa mtoto aliyefufuka acharangwa MAPANGA WATU zaidi ya 10 wasiojulikana wakiwa na mapanga na nondo waliivamia familia ya mtoto aliyedaiwa kufufuka, Shaban Maulidi kisha kuwajeruhi kwa silaha hizo watu saba, akiwemo mama mzazi wa mtoto huyo, Aziza Ramadhan, Uwazi … Read More
  • 'Miili ya magaidi yapatikana Westgate' Miili miwili iliyoungua vibaya aliyoopolewa katika eneo la kituo cha biashara cha Westgate nchini Kenya siku ya Alhamisi inawezekana kwa kiasi kikubwa ikiwa ni ya magaidi walioshambulia kituo hicho, Mbunge mmoja wa Kenya a… Read More

0 maoni: