Friday, 29 August 2014

Je unamjua Askofu bilionea Tanzania? Angalia baadhi ya picha za mikutano yake hapa.....

 ASKOFU na Nabii George David ‘Geordavie’ wa Kanisa la Geordavie Ministry ‘Ngurumo ya Upako’ lililoko jijini Arusha na Kawe.
 Hapa akionekana katika moja ya mikutano yake alipokuwa Karatu mkoani Manyara, inasemakana kuwa Askofu  Geordavie  hutoa huduma ya uponyaji kwa njia za miujiza, na mara zote huwa  na ulinzi mkali ambao haujawahi kutokea.

 Mbali  na kumiliki  chopa ambayo ameinunua , askofu huyo huambatana na msururu wa magari yenye thamani kubwa kwenye mikutano yake kiasi cha kutajwa kuwa tajiri kuliko maaskofu wengine wanatoa huduma katika makanisa ya kiroho Tanzania.

 Akiwa Karatu, mbali na ulinzi binafsi, Geordavie alikuwa akilindwa na askari wa jeshi la polisi, askari kanzu, Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na wale wa usalama barabarani.


Baadhi ya watu walikuwa wakihoji utajiri wa askofu huyo kutokana na fedha nyingi anazozitumia anapofanya mikutano katika sehemu mbalimbali jijini Arusha.
“Tunajua kuwa ni tajiri, lakini anapata wapi fedha za kutumia hivi?” alihoji muumini aliyejitambulisha kwa jina moja la Julius ambaye naye alihudhuria mkutano wa askofu huyo anayetumia kaulimbiu ya Ngurumo ya Upako katika kutoa huduma yake.


Waumini wengi wamelalamikia ugumu wanaoupata wanapotaka kumuona mtumishi huyo kutokana na ulinzi mkali anaopewa, Imefahamika kuwa  utajiri wake hakuna mfano na  nyumbani kwake Arusha, anaishi kama Mfalme Daud,” 

Related Posts:

  • Nyumba ya ‘mlawiti’yateketezwa Moshi. Wananchi wenye hasira, wameteketeza kwa moto nyumba ya mkazi wa Kijiji cha Mwika Uuwo, Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro, wakimtuhumu kulawiti wanaume  wenzake. Hasira za wananchi hao zilifikia… Read More
  • Nyani aliyejipiga picha azua mgogoro Mtandao wa Wikipidia umekataa kufuta picha ambayo Nyani ilijipiga ikisema kuwa kwa sababu picha hiyo ilipigwa na Nyani ambaye ni mnyama wala sio binadamu, basi inakuwa mali ya umma. Hii ni baada ya mpiga picha, mmiliki… Read More
  • Suarez huenda akapunguziwa adhabu  Jopo la wanasheria wanaomwakilisha mshambulizi wa Barcelona na Urugua Luiz Suarez limesema linamatumaini makubwa kuwa shirikisho la soka duniani FIFA itapunguza marufuku ya miezi minne aliyopewa mshambulizi huyo … Read More
  • BIASHARA CHAFU: Mwanafunzi chuo kikuu alazimishwa kurekodi picha za ngono “Nilipoishiwa nguvu, yule mwanamke alitoka nje na kurudi halafu alinichoma sindano yenye dawa ambayo ilinifanya nipate nguvu tena na kuendelea.  Nikapewa ratiba ya kulala na wanawake asubuhi, wavulana jioni (mashog… Read More
  • Adaiwa kumdhalilisha mfanyakazi Hai. Mkazi wa Singida Mjini, Jacqueline Kweka (30) jana alipandishwa mahakamani mjini hapa akikabiliwa na tuhuma za kumfanyia ukatili mfanyakazi wake wa ndani (15). Inadaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa akimpiga mfany… Read More

0 maoni: