Friday, 5 September 2014

Okwi: Nitacheza Simba hata bure


BAADA ya kufanikiwa kutua Simba, kiungo mshambuliaji mpya wa kikosi hicho, Mganda, Emmanuel Okwi amefunguka kuwa yupo tayari kuendelea kuitumikia klabu hiyo bure.

Okwi amesema maneno hayo akimaanisha kuwa yupo tayari kucheza bila hata kulipwa mshahara kwa kudai kuwa hilo suala la fedha siyo tatizo kwake.


Akizungumza na Championi Ijumaa, jana, Okwi ambaye amejiunga na Simba hivi karibuni akitokea Yanga na kusaini kuichezea klabu hiyo kwa miezi sita, amesisitiza kuwa anaipenda Simba na atafanya hivyo pia itakapobidi ili kulinda kiwango chake.

“Unajua sasa hivi nimebadilika na siyo Okwi yule waliyekuwa wakimjua, sitakuwa mtukutu kama ambavyo walikuwa wakinisema mwanzoni,” alisema Okwi.

Mganda huyo ameongeza kuwa anaamini yuko mahali sahihi, hivyo atahakikisha anapambana kuweka kiwango chake kuwa bora. “Nimefurahi kurejea Simba na kuitumikia timu hii, mshahara siyo tatizo,” alisema Okwi.

Kwa hisani ya Martha Mboma/GPL

Related Posts:

  • Madeni ya Harusi yamtesa CHAZ BABA! SIKU chache baada ya kufunga ndoa, Rais wa Bendi ya Mashujaa Musica, Charles Gabriel Baba ‘Chaz Baba’ ameingia kwenye mateso ya kusumbuliwa na madeni yaliyotokana na harusi hiyo. Akizungumza na mapaparazi wa Amani kat… Read More
  • WASTARA apata mguu mpya wa bandia STAA wa filamu za Kibongo, Wastara Juma Jumamosi iliyopita alikwea pipa kuelekea nchini Kenya ambako ana ziara ya siku nne kikazi na akiwa humo alipata fursa ya kupewa mguu wa bandia bure na wenyeji wake huku pia akiahidi… Read More
  • Watiwa Mbaroni dakika 3 baada ya kufnga ndoa JESHI la polisi nchini limefanikiwa kuisambaratisha ndoa ya mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari Mboga iliyopo Chalinze mkoani Pwani, Asha Daru mwenye umri wa miaka 15, aliyeozeshwa kwa Said Ally (29),… Read More
  • CHID BENZ ndani ya bifu n KASSIM WASANII wanaotamba katika muziki wa Bongo Fleva, Kassim Mganga na Rashid Makwilo ‘Chid Benz’ juzikati ilikuwa nusura wazichape baada ya kumwagiana matusi hadharani. Tukio hilo lilitokea hivi karibuni nje ya Ukumbi wa … Read More
  • Je tutafika? Watoto wadogo waoana! HAKUNA lugha inayofaa kutumika katika habari hii zaidi ya kusema hii ni kali ya mwaka! Katika hali ya kushangaza, watoto Mary Chinjendi (15) na Amos Sailowa (17), wazaliwa wa Kijiji cha Vilundilo Mbandee, Mkoa wa Dodoma, w… Read More

0 maoni: