Friday, 5 September 2014

Okwi: Nitacheza Simba hata bure


BAADA ya kufanikiwa kutua Simba, kiungo mshambuliaji mpya wa kikosi hicho, Mganda, Emmanuel Okwi amefunguka kuwa yupo tayari kuendelea kuitumikia klabu hiyo bure.

Okwi amesema maneno hayo akimaanisha kuwa yupo tayari kucheza bila hata kulipwa mshahara kwa kudai kuwa hilo suala la fedha siyo tatizo kwake.


Akizungumza na Championi Ijumaa, jana, Okwi ambaye amejiunga na Simba hivi karibuni akitokea Yanga na kusaini kuichezea klabu hiyo kwa miezi sita, amesisitiza kuwa anaipenda Simba na atafanya hivyo pia itakapobidi ili kulinda kiwango chake.

“Unajua sasa hivi nimebadilika na siyo Okwi yule waliyekuwa wakimjua, sitakuwa mtukutu kama ambavyo walikuwa wakinisema mwanzoni,” alisema Okwi.

Mganda huyo ameongeza kuwa anaamini yuko mahali sahihi, hivyo atahakikisha anapambana kuweka kiwango chake kuwa bora. “Nimefurahi kurejea Simba na kuitumikia timu hii, mshahara siyo tatizo,” alisema Okwi.

Kwa hisani ya Martha Mboma/GPL

Related Posts:

  • Soma habari kamili ya Bibi Harusi aliyeaga dunia dakika 30 kabla ya kufunga ndoa Bi harusi huyo, Levina Mmassy (23) aliyekuwa mkazi wa Chanika, Handeni mkoani Tanga alifariki dunia Jumamosi ya Julai 6, mwaka huu, majira ya mchana, muda mfupi kabla ya kufunga ndoa na Kasisi Masawe. PADRI ASUBIRI Tuki… Read More
  • Dida apigwa dongo BAADA ya hivi karibuni Mtangazaji wa Radio Times, Khadija Shaibu ‘Dida’ kufunga ndoa na mwanaume aitwaye Ezden, mashosti zake wamemtaka kutulia sasa na asijaribu kugeuza ndoa kuwa fasheni. Wakizungumza na Ijumaa kwa… Read More
  • NGASSA akata Mzizi wa Fitina...... atua Mazoezini Yanga HATIMAYE kiungo mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa (pichani), amekata mzizi wa fitna baada ya kuanza kujifua rasmi na timu hiyo, ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu asajiliwe. Awali kulikuwa na utata wa mchezaji huy… Read More
  • Changudoa anayewatesa Polisi Dar...... MREMBO mwenye ulemavu wa ngozi, Emmily Omari, 23, mkazi Buguruni, Dar anayedaiwa kujihusisha na biashara haramu ya uchangudoa, hivi karibuni alipandishwa kizimbani kwa madai ya kufanya kosa hilo. Emmily ambaye amekuwa aki… Read More
  • Wema Sepetu matatani tena? DIVA wa filamu za Bongo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu anasakwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, Dar es Salaam kwa tuhuma za kufanya fujo hotelini, kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga makofi meneja wa h… Read More

0 maoni: