Friday, 23 August 2013

Yanga wamuongezea adhabu Mrisho Ngassa?

IMEFAHAMIKA kuwa Klabu ya Yanga, ndiyo iliyochangia ukubwa wa adhabu aliyopewa kiungo wake mshambuliaji Mrisho Ngassa, Championi Ijumaa limebaini. Taarifa hiyo inakuja wakati ambao Ngassa amefungiwa kucheza mechi sita za mashindano pamoja na kuilipa Simba jumla ya shilingi milioni 45, sababu kubwa ikiwa ni kusaini mikataba miwili, ule wa Yanga na ule wa Simba.
Boniface Wambura ambaye ni Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ameliambia Championi Ijumaa kuwa, adhabu ya kufungiwa michezo sita kwa Ngassa imewekwa maalum, kutokana na Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji kutaka mchezaji huyo apate uchungu wa makosa aliyoyafanya na siyo kutegemea kulipiwa na klabu.
Wambura alisema adhabu hiyo imetokana na kasumba ya klabu mbalimbali ambazo zimekuwa zikiamua kulipa faini wanazokatwa wachezaji wao kwa makosa mbalimbali, maamuzi ambayo yanasababisha wachezaji kurudia makosa hayo.
“Adhabu kama hii ni maalum kuweza kumfanya mchezaji aone makali ya kosa alilofanya ili asiweze kurudia wakati mwingine, kamati imebaini kuwa makosa kama haya kila wakati yanakuwa yakijirudia kwa kuwa klabu ndizo zinazosababisha hilo,” alisema Wambura na kuongeza:
“Hata huku TFF, tunaona jinsi klabu zinavyofanya, endapo mchezaji fulani anapofanya makosa na kuhukumiwa utaiona klabu ndiyo inakuja na kuilipa faini husika, maamuzi kama hayo yanasababisha mchezaji asijue makali ya makosa anayofanya, ndiyo maana adhabu hii ikawa kali zaidi.”

Kwa hisani ya Khatimu Naheka/GPL

Related Posts:

  • KASEJA atua YANGA Mlinda mlango nambari moja nchini Tanzania kwa kipindi kisichopungua miaka 10 mfululizo Juma Kaseja Juma jana majira ya saa 2 usiku alisaini mkataba wa kuitumikia klabu ya Young Africans yenye makao yake Twiga/Jangwani kwa… Read More
  • Rice agundulika kuwa na saratani Mchezaji wa zamani wa timu ya Ireland kaskazini na mlinzi wa zamani wa Arsenal Pat Rice amefikishwa hospitalini baada ya kugundulika kuwa na ugonjwa wa Saratani. Rice mwenye umri wa miaka 64 aliichezea mara 528 timu ya w… Read More
  • MTOTO wa kwanza wa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage amelazwa mahututi katika hospitali iliyoelezwa kuwa katika Mji wa Atlanta nchini Marekani. Taarifa za kulazwa kwa mtoto huyo wa kwanza wa Rage ambaye jina … Read More
  • Mike Tyson 'returns Evander Holyfield's ear' 16 years after infamous bite fight in Foot Locker commercial Making amends: The Footlocker commercial sees Mike Tyson return Evander Holyfield's ear with a remorseful look on his face Surprise visit: Evander looks lost for words when he sees Tyson turning up at his door … Read More
  • Ally Badru na Awadhi Issa watua Msimbazi Wazee wa Msimbazi , Simba Sports Club  jana imewasajili wachezaji wawili  toka Mtibwa Sugar na Canal suez ya Misri........ Habari zilizotufikia wadaku wa mji zinasema wachezaji hao ni Awadh Issa wa Mtibwa Sugar n… Read More

0 maoni: