People's Magazine
The place where you can find everything...
Home
Saturday, 8 December 2012
Home
»
Celebrities News
,
Magazeti pendwa
» UKIMWI HUOO!
UKIMWI HUOO!
By
Unknown
21:41
No comments
KINACHOONEKANA kwa sasa Bongo ni ugumu wa serikali kupambana na vita dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi baada ya jamii kushindwa kubadilika na kuona ugonjwa huo ni wa kawaida kama ilivyo kukohoa au kichwa kugonga.
Hilo limedhihirika baada ya juzi chanzo chetu cha habari kupasha kwamba, baadhi ya wafanyabiashara na wabunge wameingia ‘kazi’ ya kuwanasa mastaa wa kike Bongo, hasa waigizaji wa filamu.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, wafanyabiashara maarufu wa jijini Dar na baadhi ya waheshimiwa wabunge wamekuwa wakiwaibukia mastaa wanapokuwa kambini wakirekodi filamu na kuwahonga fedha nyingi sanjari na kuwanunulia magari ya kifahari ya kutembelea.
MCHEZO UPO HIVI
Inadaiwa wanachofanya baadhi ya mastaa, hasa wakiwa kambini, hupiga picha chafu (angalia picha ukurasa wa mbele) wakiamini zina mvuto na kuzitundika BBM kwenye simu zao ambapo wafanyabiashara na wabunge hao wanapoziona huweweseka na kuanza msako wa kuwapata.
Chanzo kilisema: “Zamani mapedeshee ndiyo walikuwa wanaongoza kwa kuwachukua mastaa wa kike kwa kutumia picha za mitandaoni na kwenye magazeti, siku hizi mastaa wenyewe wamewashtukia, hawawataki mapedeshee, wanasema fedha zao ni za msimu.
“Siku hizi mastaa wakiwa kambini hupiga picha za hasarahasara na kuzitupia BBM, wafanyabiashara na wabunge wakiziona wanakimbilia kupanga foleni kwenye mahoteli ambayo mastaa hao wamepiga kambi.”
Aidha, chanzo kikasema kuwa baadhi ya wafanyabiashara huhonga kuanzia shilingi 1,000,000 hadi 5,000,000 kama staa ana jina kubwa.
“Kama staa ana jina kubwa, anaweza kuhongwa kuanzia milioni moja hadi tano, kama ni supastaa kama Wema, Wolper, Odama, Rose Ndauka hawa wanaweza kuhongwa hata magari ya kifahari,” kilisema chanzo hicho.
MASTAA WANAVYOTUMIKA
Chanzo kikasema kuwa, mbaya zaidi wanaume hao wamekuwa wakigoma kufanya mapenzi kwa kutumia kinga (kondom) kwa madai kwamba, hawawezi kuhonga pesa nyingi halafu kitandani wakatumia kondom kwani wanakosa raha.
“Kinachouma zaidi ni kwamba, hao wanaume wakiwachukua mastaa hadi chumbani wanakataa kutumia kondom, madai yao pesa wanazohonga ni ndefu (nyingi) kwa hiyo ni afadhali wafaidi, wanasahau kwamba Ukimwi upo.
“Kwa sababu ya tamaa ya pesa, dada zetu (mastaa) wanashindwa kuwa na msimamo wa kutumia kondom. Anaweza kukataa sana, lakini mheshimiwa anaahidi kumnunulia gari, hapo ndipo masharti yanalegezwa,” kilisema chanzo.
BAADA YA KUCHUJA KINACHOFUATA…
Chanzo kikasema kumekuwa na vilio na kusaga meno kwa baadhi ya mastaa kwani wanaponunuliwa magari, kadi zinakaa kwa wanaume hao, baadaye wanawanyang’anya.
“Mbaya zaidi, wapo mastaa waliwahi kushawishika na kutoa penzi bila kinga kwa ahadi ya kununuliwa gari, waliponunuliwa hawakupewa kadi ya kumiliki, baadaye wakanyang’anywa,” chanzo kilitoboa.
WASEMAVYO MASTAA
Baadhi ya mastaa waliozungumza na paparazi wetu walikiri kuwepo kwa wanaume wenye tabia hiyo, lakini kila mmoja akasema yeye haijamtokea.
Wolper: “Ni kweli, wapo wanaume wanabembeleza sana kutotumia kondom na kuahidi fedha au gari, lakini kama staa anakubaliana na ombi hilo ni kujiangamiza, Ukimwi unaua. Ila mimi sijawahi kukutana na mwanume wa hivyo, kwanza nilishasema ndani ya gari natembea na kondom.”
Jack wa Chuz: “Wewee, uamuzi wa kufanya hivyo ni wa mtu mwenyewe na umri wangu huu nikubali kufanya mapenzi bila kinga kwa sababu ya gari? Kwani gari kitu gani bwana.”
Nisha: “Mh! Nimewahi kusikia kuna wasanii waliingia kwenye mtego huo na sasa wanajuta maana hawana uhakika na afya zao, kwenda kupima wanaogopa, magari walishanyang’anywa, mimi aku!”
Flora Mvungi: “Mimi siwezi kusema kitu maana nina wangu, kama ni gari au pesa ananipa yeye, pole yao ambao hawajajipanga hadi leo.”
Aidha, chanzo kilisema kuwa, maeneo hatari ya kufanyika kwa michezo hiyo ni hoteli kubwa ambazo wasanii hupiga kambi kwa ajili ya kurekodi filamu.
Kwa hisani ya GLP
Email This
BlogThis!
Share to X
Share to Facebook
Categories:
Celebrities News
,
Magazeti pendwa
← Newer Post
Older Post →
Home
0 maoni:
Post a Comment
Social Profiles
Popular
Tags
Blog Archives
Search this Blog
Baby who had the most misshapen head doctors had ever seen undergoes pioneering surgery to stop her brain from being squashed
Kaydence Theriault and her fellow triplets Taylor and Kaylin were all born with Crouzon Syndrome, which causes the head to become misshapen...
Sad News: Actress Ini Edo Suffers Miscarriage After Six Years Of Marriage
Reports have it that beautiful actress, Ini Edo, has suffered another miscarriage making her thirdmiscarriage in her husband’s house, ...
Baada ya kufunga ndoa kimyakimya sasa Rais wa Masharobaro aitwa baba...
'I want to look in the mirror and see I'm not the same': Haitian teen has FOUR-POUND tumor removed from her face
WARNING: GRAPHIC IMAGES BELOW Hennglise Dorvial, 15, had the tumor removed during surgery that took 12 hours Surgery organized and paid ...
Diamond ndani ya penzi jipya?
Ni jana tu, Raisi Wa Wasafi, Diamond Platnumz alitupia picha katika moja ya mitandao ya jamii anayotumia, huu ukiwa ni Instagram ya mtang...
Gari ndogo aina ya Nissan Terano lenye nambari za usajili T 332 AKK
UKIMWI HUOO!
KINACHOONEKANA kwa sasa Bongo ni ugumu wa serikali kupambana na vita dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi baada ya jamii kushin...
Vivazi vya kutokea hivi hapa ................
Urembo kazi? Kim ajipata damu yake usoni
Baby on the way?
Mtoto muda wowote kuanzia sasa - Mama mtarajiwa akiwa sambamba na baba mtarajiwa katika mitaa ya Hollywood jana
Powered by
Blogger
.
My favorite News blog
Loading...
Celebrities Gossip
Loading...
.
Tags
Afya
(116)
Broken heart stories
(1)
Celebrities kids
(18)
Celebrities News
(783)
Children
(4)
Death Anouncement
(1)
Dini
(27)
Elimu
(5)
Extraordinary People
(12)
Familia
(26)
Full aibu
(87)
General
(20)
Karibu Jamvini
(1)
Katuni
(11)
Kazi za Jamii
(3)
Magazeti pendwa
(228)
Mahusiano
(281)
Majanga
(16)
mambo ya kuiga
(3)
Mapishi
(2)
Michezo na Burudani
(49)
Mikasa ya Maisha
(2)
Mila na desturi
(14)
Moyo Mpweke
(3)
Msaada kwenye tuta...
(10)
Nyumba
(28)
OMG
(476)
OMG... Black are beautiful
(10)
Picha huongea
(25)
Sayanzi na Tekinolojia
(3)
Siasa
(82)
Tangazo
(2)
Tiba Mbadala
(4)
True story
(77)
Ugaidi
(1)
Ukatili
(55)
umaarufu kazi
(28)
Urembo
(20)
Video
(10)
Vipaji
(3)
Vituko mtaani
(164)
Vivazi na Mitindo
(171)
Wanaume
(32)
Wanawake
(121)
0 maoni:
Post a Comment