Friday, 31 May 2013

FA & JAYDEE waahirishwa show zao kutokana na kifo cha Magwea...

KUTOKANA na habari za kufariki kwa Albert Mangwair ‘Ngwea’, msanii ambaye ni mmoja kati ya wana Hip Hop maarufu nchini, Hamis Mwinjuma ‘MwanaFA’ ametangaza kuahirisha shoo yake ya The Finest iliyokuwa ifanyike leo (Ijumaa). 

MwanaFA amesema ameamua kufanya hivyo ili kupisha maombolezo ya msanii huyo maarufu, baada ya hapo atatangaza siku nyingine ya kufanya shoo hiyo.

“Nawaomba radhi mashabiki wangu hasa waliokata tiketi, wawe na subira kwani hili limetokea na ni letu sote. Tarehe ya shoo tutaitangaza baada ya mwili wa marehemu kupumzishwa kwenye nyumba ya milele,” alisema msanii huyo.

Aidha, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ naye ameahirisha shoo yake ya kutimiza miaka 13 tangu alipoanza gemu la muziki ambayo ingeenda sambamba na uzinduzi wa albamu yake iitwayo Nothing But the Truth iliyokuwa ifanyike leo.

Kwa hisani ya GLP

Related Posts:

  • Dunia ina mambo !......Kijana wa miaka 32 answa na kibibi kizee cha miaka 80 Tukio hilo la kustaajabisha limetokea mwishoni mwa wiki iliyopita, nyumbani kwa bibi huyo, Yombo –Buza, jijini Dar es Salaam ambapo wajukuu wa bibi huyo ndiyo waliomnasa. Kwa mujibu wa chanzo chetu, wajukuu wa bibi hu… Read More
  • Jeuri ya fedha: Mke anunua TALAKA kwa milioni 4 Maharusi katikati wakiwa katika picha ya pamoja na wazazi wa bibi harusi (kushoto) na wazazi wa bwana harusi (kulia). UNAWEZA kusema ni jeuri ya fedha baada ya  mwanamke, Rukia Apach kukubali kulipa shilingi milion… Read More
  • Ndoa ya THEA and MIKE yavunjika? SIKU chache baada ya ndoa ya mwigizaji, Ndubagwe Mithayo ‘Thea’ kuvunjika, mwigizaji Deogratius Shija ‘Shija’ ameibuka na kueleza maumivu anayoyapata juu ya tukio hilo. Akizungumza na Amani hivi karibuni, Shija alisem… Read More
  • RAY, CHUCHU HANS laivuuuu AMA kweli penzi ni kikohozi kulificha huwezi! Hatimaye uliokuwa uhusiano wa chini kwa chini wa nyota wawili wa sinema za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ na Chuchu Hans, siyo siri tena baada ya wahusika hao wakuu kujiachia ‘l… Read More
  • Kope za bandia zampofua macho mrembo AMA kweli hujafa hujaumbika, mrembo Khadija Omar, mkazi wa Kigogo, Dar amepata pigo kufuatia kupofuka macho alipokuwa akiwekwa nyusi bandia katika saluni moja iliyopo maeneo hayo, Risasi Jumamosi lina mkasa … Read More

0 maoni: