Tuesday, 15 January 2013

Konda wa Daladala auwawa kikatili Dar ...

KIJANA mmoja, Twaha Ally (36 - pichani) ambaye alikuwa kondakta wa daladala linalofanya safari zake kati ya Majohe nje kidogo mwa Jiji la Dar es Salaam  na Gongo la Mboto ameuawa mwishoni mwa wiki iliyopita na watu wasiojulikana waliomvamia na kumnyang’anya fedha.  Marehemu alikutwa na mauti  hayo baada ya kushambuliwa na watu hao kituo cha daladala baada ya kugoma  kutoa fedha ambazo walitaka  awepe.

Taarifa kutoka eneo  la tukio Gongo la Mboto, zinasema kuwa Twaha baada ya kufika kituoni hapo alishuka  kwa lengo la kwenda kununua sigara lakini alishitukia anazingirwa na watu asiyowajua wakimtaka awape fedha.

 Aidha, inadaiwa wakati wa purukushani ya kumnyang’anya fedha, wapita njia walidhani ni watu waliotaniana lakini walishituka baada ya kijana huyo kuchomwa na kitu chenye ncha kali.

Shuhuda mmoja ambaye hakupenda jina lake kuandikwa gazetini alimueleza mwandishi wetu kuwa mara baada ya Twaha kuchomwa mwilini na vitu vyenye ncha kali, dereva wa basi alilokuwa akifanyia kazi alimpigia simu jirani yake na kumfahamisha kuhusu tukio hilo kushambuliwa.

 Kwa kuwa Twaha alikuwa amefariki, alimfahamisha jirani huyo asiwaambie ndugu zake kwani angewachanganya. Hadi sasa haijajulikana marehemu alinyang’anywa  kiasi gani  cha fedha. Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Kipolisi Ilala,  ACP Marietha Minangi alikiri kutokea kwa tukio hilo na kwamba watu 28 walikamatwa, watatu wanadaiwa kuhusika na tukio hilo.

Kamanda huyo alisema msako huo ulifanywa kwa kushirikiana na polisi jamii na uongozi wa serikali ya mtaa huo na kuongeza kuwa zoezi hilo la kusaka wahalifu linaendelea.


Kwa hisani ya http://www.globalpublishers.info

Related Posts:

  • Majambazi yavamia gari na kupora milioni 40 Majambazi yaliyokuwa na silaha aina ya SMG yakiwa na pikipiki aina ya Bajaj Boxer yamevamia gari ndogo aina ya Toyota Vitz yenye no za usajili - T929 CCX (pichani juu) leo mchana katika  eneo la Sayansi… Read More
  • Sheha wa Tomondo omamwagiwa Tindikali Zanzibar Jana usiku mtu asiyejulikana alimvamia Sheha wa Tomondo Mohammed Omary Said (pichani) na kumwagia Tindikali sehemu za uso na kifua na kumsababishia  majeraha na maumivu makali, tukio hilo lilitokea jana usiku wakati S… Read More
  • I'll kill myself': Escaped child bride, 11, explains why she ran away from home Nada al-Ahdal was saved from the forced engagement by her uncle He told her suitor that she 'was no good for him and did not wear a veil'  The practice of marrying young girls is widespread in Yemen A harrowing vi… Read More
  • Mtanzania auwawa Marekani POLISI wametambua mwili wa mwanafunzi wa Howard University aliyeuawa kwenye jaribio la uhalifu Alhamisi usiku. Omar Sykes, 22 (pichani), na mwanafunzi mwenzake walikuwa wanatembea maeneo ya 700 block of Fairmont S… Read More
  • Mzee wa KANISA azikwa hai KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida wananchi wa kijiji na kata ya Mkwajuni Wilaya ya Chunya Mkoani hapa wamemzika Mwanakijiji mwenzao akiwa hai wakimtuhumu kusababisha kifo cha Mkazi mmoja kijijini hapo. Tukio hilo la k… Read More

0 maoni: