Saturday 15 December 2012

Jokate kuolewa mwakani?

MWANAMITINDO Jokate Mwigelo ‘Kidot’ ameona umuhimu wa kuingia kwenye maisha ya ndoa baada ya kuibuka na kudai kuwa, mwakani na yeye ataolewa. Akizungmza na Ijumaa hivi karibuni kuhusiana na malengo yake kwa mwaka ujao, Jokate alisema kuwa, miongoni mwa mambo makubwa aliyopanga kuyatimiza ndani ya mwaka huo ni kuolewa.
“Kikubwa ambacho nafikiria kukitimza mwakani endapo Mungu atanijaalia uzima ni kuolewa ili nami niwe mke wa mtu, atakayenioa kwa sasa ni siri yangu na itakuwa ni ‘sapraizi’ kwa wengi,” alisema Jokate.

Jokate amewahi kuripotiwa kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mcheza mpira wa kikapu, Hasheem Thabit na pia ikavuma kuwa ametoka na mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ ila mpaka sasa haijulikani kajiweka kwa nani kutokana na mdada huyu kuwa msiri sana.

0 maoni: