Saturday 15 December 2012

Makosa wayafanyayo wanaume wawapo kitandani na mpenzi mpya...!



Linapokuja swala la kujamiiana kwa wapenzi wapya ambao hawajawahi kukutana kimwili tangu kujuana kwao ni mtihani mkubwa. Kwani kila mmoja anakuwa na matarajio tofauti na mwenzake. Yaani hakuna anayejua kwa usahihi kwamba mwenzake anapenda afanyiwe nini ili kupata ashki ya kushiriki jambo hilo, lakini wanawake wengi ndio ambao hulichukulia jambo hilo kwa uzito mkubwa kiasi kwamba, kama mwanaume asipomudu kuwa mtundu kitandani, nafasi yake kwa mwanamke huyo inaweza kuwa finyu sana labda tu kama atakuwa amempendea pesa…Hapa chini nitaeleza makosa yanayoonekana madogo yanayofanywa na wanaume kitandani wakutanapo na wapenzi wapya ambayo wanawake huyapa uzito mkubwa:


1. Kumuandaa 

Kumuandaa mwananamke sio pale muwapo kitandani tu, la hasha, maandalizi huanzia katika mazungumzo ili kumuweka katika mood. Hapa mwanaume anatakiwa aongee na mpenzi wake kwa lugha nzuri, kwa maneno matamu na yenye mahaba. Atumie muda mwingi kuzungumza naye, asiwe na haraka kuanza kufanya tendo. Mazungumzo yahusu masuala ya uhusiano ukiwemo upendo. Busu lililotulia na sio la papara linatajwa kuamsha hisia za mwanamke kushiriki tendo, lakini pia mwanaume anashauriwa kuwa msomaji mzuri wa hisia za mwanamke ili kujua ni eneo gani akimgusa kwa kumpapasa mwili wake unasisimka. Kwa mwanamke kufanya mapenzi sio kile kitendo cha kuingiliwa, bali ni kitendo cha kumuandaa kiakili na kimwili ili awe kwenye mood ya kushiriki jambo hilo. iwapo mwanaume akili yake itakuwa inalenga tu kile kilichopo katikati ya mapaja ya mwanamke na labda matiti yake, basi hapo mwanamke atamuona sio kabisa, yaani hatoweza kumfikisha kileleni.

2. Unadhifu

Hakuna kitu kinachowakera na kuwakwaza wanawake kama mwanaume mchafu hususan wakati wa kujamiiana. Hilo linaweza kumfanya mwanamke asifikirie tena kufanya tendo na mwanaume huyo. Unakuta mwanaume ananuka kikwapa au amevaa chupi wiki nzima bila kuifua na akiivua eneo la chini ya kitovu lote linanuka au ana kucha ndefu tena chafu na zina ncha kali kwenye kona (sharp edge) kiasi kwamba akimpapasa mwanamke zinamkera badala ya kumpa ashki. Akipumua mdomo unanuka, yaani akimpiga busu mwanamke anamkata stimu yote ya kufanya tendo hata kama alikuwa tayari. Inashauriwa mwanaume kuoga na kupiga mswaki kama hana uhakika na harufu ya kinywa chake, la sivyo anaweza kutumia chewing gum za kuondoa harufu mbaya mdomoni kabla ya kukutana na mwanamke na pia kukata kucha na kuondoa ncha kali zile zinazojitokeza pembeni ya ukucha ili zisimkere mwanamke wakati wa kumuandaa……

3. Mapenzi ya vurugu na yenye kuumiza

Tukiacha tatizo la kukerwa na harufu na kucha, lakini pia wanawake hawapendi mwanaume anayetwanga nje ndani wakati wa kufanya mapenzi kama vile anachimba dhahabu. Wanawake wanapenda mitwango yenye staha. halafu itokee mwanaume huyo awe ana kucha ndefu zenye ncha zilizojitokeza pembeni, kisha awe anautumia mkono wake kumpapasa mwanamke sehemu mbalimbali za mwili wake huku akiendelea kutwanga kwa fujo……..Aaaaaaagh!! 

Asije akatarajia mwanamke huyo akatamani tena kujaamiana naye, labda kuwe na kitu kingine anachokitafuta kwa mwanaume huyo na siyo mapenzi. Kuna baadhi ya wanaume hupenda kuchezea chuchu za maziwa wakati wa kufanya mapenzi kwa kuziminya kwa nguvu au kung’ata maeneo mbalimbali ya mwili wa mwanamke kwa nguvu. Mwili wa mwanamke uko laini laini na unatakiwa ashikweshikwe kwa makini na kwa staha. Hakuna ubaya kumng’ata ng’ata mwanamke kimapenzi (love bite) hapa na pale lakini inashauriwa kuchunguza kama anafurahia kitendo hicho kwa kumwagalia usoni, akiona anaonyesha sura ya kukereka kwa maumivu, basi inashauriwa kuacha na kubadilisha kwa kujaribu kitu kingine kwani wanawake wana maeneo mengi sana ya kuamsha ashki, na akimpatia atamsikia mwenyewe akiweka msisitizo kwamba aendelee……

4. Kimya mno ….. Au kupiga makelele 

Wanaume wengi hupenda sana mwanamke anapopiga makelele pale wafanyapo mapenzi lakini pia wanawake hupenda kuona kama mwanaume naye anafurahia tendo kama anavyofurahia yeye anavyofurahia. kama mwanaume ni mkimya anapofanya mapenzi yaani haongei chochote yeye anatwanga tu, mwanamke anaweza kujiuliza kama mwanaume huyo anafurahia tendo au la. Wakati mwingine ile sauti ya kupumua kwa sauti itolewayo na mwanaume wakati wa kufanya mapenzi inaweza kuwaridhisha baadhi ya wanawake, lakini wengine wanapenda kusikia mazungumzo kutoka kwa mwanaume. Iwapo mwanaume atapotelewa na maneno kutokana na kusikilizia utamu wa tendo inashauriwa japo ataje jina la mwanamke hata mara chache ili kumfanya mwanamke ajue kuwa akili na mawazo ya mwanaume huyo yapo kwake.

Hapa naomba kuweka angalizo…. kama mwanaume ni mtu wa kuongea sana wakati wa kufanya mapenzi anaweza kumpotezea mwanamke umakini wa kuvuta hisia ili kufika kileleni. Kwani kuna baadhi ya wanaume huwauliza wanawake wanaofanya nao mapenzi maswali mengi yasiyo na maana.. “Unauonaje huu mtindo.” “Unajisikiaje nikikushika hapa.” “Je ninafanya vizuri na huumii.” Lo lo lo lo loooooo….Huna haja ya kuuliza maswali yote hayo, kwani mwili wake unakupa ushirikiano sasa maswali yote hayo ya nini….! Najua hakuna ubaya kumuuliza mwanamke kama anajisikiaje au kama unavyofanya ni sahihi kwa maana kama mtindo unaotumia haumuumizi, lakini hilo hufanyika katika hatua ya mwanzo, sio pale mchezo umekolea unaanza kuuliza maswali, unakuwa unamkera tu…… Funga mdomo wako na uendelee na shughuli.

5. Kulazimisha Oral Sex

Nikisema orol sex, nadhani mnaelewa. Kuna baadhi ya wanaume hupenda kuchezewa sehemu za siri au kunyonywa. Si vyema kumlazimisha mwanamke kunyonya bila ridhaa yake. Kama anapenda kufanya hivyo mwache aamue mwenyewe na sio umshike tu kichwani na kumuelekeza yalipo maumbile yako. Kama mwanamke anapenda kufanya hicho kitendo mwache afanye mwenyewe na hahitaji kuelekezwa..


6. Kumaliza haraka au kuchelewa kumaliza

Najua wanaume watasema “hii ni ‘too much.’ Kumaliza haraka ni shida na kuchelewa kumaliza pia ni shida, sasa tushike lipi…..!”Nataka muelewe, kama inakuchukua dakika mbili kumaliza, hilo ni tatizo kaka yangu, katafute msaada wa kitabibu uondokane na fedheha kabla ya kuparamia mwanamke. Kwa wanawake wengine inaweza isiwe ni tatizo iwapo utamuandaa vizuri kabla ya kumuingilia ili kama ni kumaliza mmalize pamoja hivyo kutogundua tatizo lako labda..! lakini kama sio mzuri katika kumuandaa mwanamke, linaweza kuwa tatizo na ukajikuta anakudharau baada ya kumaliza tendo… (Najua kwamba siku ya kwanza kukutana na mpenzi mpya inaweza kukufanya ukamaliza haraka kutokana na kuhemkwa, lakini basi jitahidi mara ya pili uende sawa usije ukamaliza haraka tena…..).

Lakini pia wanawake hawakuumbwa kwa ajili ya mashindano ya mbio za kufanya mapenzi. Nakubali kwamba wapo baadhi ya wanawake wanahitaji muda zaidi ili kufika kileleni. Lakini kama itachukua dakika 45 mpaka saa moja bado unatwanga tu, angalia usije msababishia mwenzio michubuko katika sehemu zake za siri. Inatakiwa kuonyesha ushirikiano katika jambo hilo zaidi ya kujipendelea mwenyewe……!

7. Hutupi kifanyio baada ya kumaliza…!

Kutupa kondom uliyotumia wakati wa kufanya mapenzi ni kazi yako na si kazi yake. Sio uungwana umemaliza kufanya naye mapenzi kisha unamwagiza akatupe kondom uliyotumia. Lakini pia sio busara kuiweka chini na kuiacha ikichafua sakafu. Haijalishi mko guest house, nyumbani kwako au kwa mpenzi wako, kinachotakiwa ni kuonyesha ustaarabu. Ni nyema ukaivua na kuiviringisha kwenye toilet paper, karatasi au kipande cha gazeti na kuiweka mahali pazuri kabla ya kwenda kuitupa mahali panapostahili………. Vinginevyo mpenzi wako atakuona wewe sio msafi na siyo mstaarabu………….

0 maoni: