Friday, 14 December 2012

Baby Madaha aumbuka! Adaiwa kodi ya nyumba ya miaka 3 ! apewa notice ya siku 2 ............

 
Wambeya wa mji tumezinyaka  taarifa za kusikitisha kuhusu msanii wa muziki wa kikazi kipya - tunda la Bongo Star Search Baby Madaha ....... Inasemekana Baby Madaha kapewa notice ya siku 2 na mwenye nyumba wake  na hii yote imetokana na msanii huyo kulimbikiza deni kwa muda wa miaka 3 kinachokadiriwa kufikia kiasi cha shilingi milioni 2 za kitanzania hadi sasa!!!


Nasikia Baby madaha kila siku alikuwa anampa  sound mwenye nyumba wake mara oooh nitakupa  kesho  mara wiki ijayo hali iliyomfanya mwenye nyumba huyo  kuchoka na kumpa notice ya siku 2 ili awe amelipa deni hilo.... kama haitoshi msanii huyo hajaonekana nyumbani hapo maeneo ya Kinondoni kwa siku tatu, na taarifa za notice katumiwa kwa njia ya kilongalonga - simu. 

Inasemekana Baba mwenye nyumba aligadhibika kinoma kiasi  cha kutaka kutoa vitu vya msanii huyo nje lakini kutokana na uvumilivu wake aliacha na aliamua kumpigia simu kuwa anampa siku mbili awe amelipa kiasi hicho cha pesa bila hivyo aondoe vitu vyake.
 


Wambeya hawakukubali wakavuta uzi na kumpata Baby  Madaha na alikuwa na haya ya kusema - Ni kweli taarifa za notice nimezipokea kwa njia ya simu ila hiyo habari ya  kutolala ndani ni ishu ya uongo! Baby aliongeza na kusema sijashindwa kulipa hela hizo lakini nilikuwa na mipango yangu naifanya kwani siwezi kudhalilishwa kwa pesa ndogo kiasi hicho hata kama anaishi kwenye nyumba ya kupanga.

Related Posts:

  • Achezea kichapo kwa kufanya mapenzi karibu na Msikiti........... KHAAA! Operesheni Fichua Maovu ‘OFM’ iliyo chini ya Global Publishes, ipo mzigoni na hivi karibuni imenasa tukio la aina yake ambapo mke wa mtu amechezea kichapo ‘hevi’ akidaiwa kufanya ukahaba jirani na msikiti, Risasi Mc… Read More
  • Mtaa wa ngono wafumuliwa.... NI hakika ‘mtaa wa ngono’ umefumuliwa! Sakata hilo lilijiri saa tisa usiku, Ijumaa iliyopita, Barabara ya Shekilango, kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori jijini Dar eneo ambalo makahaba wameligeuza chumbani, Operesheni Fichua M… Read More
  • ISHA MASHAUZI mbaroni kwa wizi MWIMBAJI ambaye pia ni bosi wa Kundi la Mashauzi Classic, Aisha Ramadhan Makongo ‘Mashauzi’, Jumatano iliyopita alikumbwa na masaibu mazito kufuatia kudakwa na polisi wa Kituo cha Msimbazi, Dar akituhumiwa kukwapua mk… Read More
  • Msanii wa ZE COMEDY afanya uchafu beach MSANII memba wa Kundi la Ze Comedy linaloruka kupitia Runinga ya East Africa, Master Face amenaswa akifanya uchafu wa kushikana ‘kimalovee’ na msanii mwenzake aitwaye Happy ambaye alikuwa ametinga kivazi cha nusu utupu. … Read More
  • Mrembo afukuzwa jukwaani kwa kuvaa nusu uchi...... MWENYEKITI wa Kamati ya Mashindano ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga Jumamosi iliyopita alimtimua mshiriki wa shindano la Redd’s Miss Morogoro 2013, Saphina Chumba- pichani (20) jukwaani wakati shindano hilo lilipokuwa li… Read More

0 maoni: