Friday, 14 December 2012

Baby Madaha aumbuka! Adaiwa kodi ya nyumba ya miaka 3 ! apewa notice ya siku 2 ............

 
Wambeya wa mji tumezinyaka  taarifa za kusikitisha kuhusu msanii wa muziki wa kikazi kipya - tunda la Bongo Star Search Baby Madaha ....... Inasemekana Baby Madaha kapewa notice ya siku 2 na mwenye nyumba wake  na hii yote imetokana na msanii huyo kulimbikiza deni kwa muda wa miaka 3 kinachokadiriwa kufikia kiasi cha shilingi milioni 2 za kitanzania hadi sasa!!!


Nasikia Baby madaha kila siku alikuwa anampa  sound mwenye nyumba wake mara oooh nitakupa  kesho  mara wiki ijayo hali iliyomfanya mwenye nyumba huyo  kuchoka na kumpa notice ya siku 2 ili awe amelipa deni hilo.... kama haitoshi msanii huyo hajaonekana nyumbani hapo maeneo ya Kinondoni kwa siku tatu, na taarifa za notice katumiwa kwa njia ya kilongalonga - simu. 

Inasemekana Baba mwenye nyumba aligadhibika kinoma kiasi  cha kutaka kutoa vitu vya msanii huyo nje lakini kutokana na uvumilivu wake aliacha na aliamua kumpigia simu kuwa anampa siku mbili awe amelipa kiasi hicho cha pesa bila hivyo aondoe vitu vyake.
 


Wambeya hawakukubali wakavuta uzi na kumpata Baby  Madaha na alikuwa na haya ya kusema - Ni kweli taarifa za notice nimezipokea kwa njia ya simu ila hiyo habari ya  kutolala ndani ni ishu ya uongo! Baby aliongeza na kusema sijashindwa kulipa hela hizo lakini nilikuwa na mipango yangu naifanya kwani siwezi kudhalilishwa kwa pesa ndogo kiasi hicho hata kama anaishi kwenye nyumba ya kupanga.

Related Posts:

  • TIMBWILI : MUME wa mtu nusura auawe na KIMADA WAKATI Oparesheni Fichua Maovu katika jamii inayoendeshwa na Global Publishers ikiwa kazini, wikiendi iliyopita ilinasa timbwili ‘hevi’ la aina yake kwa mwaka 2013 ambapo mume wa mtu, Joseph Hussein (31), nusura auawe n… Read More
  • Mambo ya Chuma ulete yamtokea MREMBO puani.... MREMBO mmoja, Rukia Omari mkazi wa Mbezi Beach jijini Dar amebambwa akidaiwa kuiba fedha kwa njia za miujiza eneo la  Bunju Mwanjenje kwenye duka la Wapemba. Imeelezwa kuwa katika tukio hilo, Rukia alichukua fed… Read More
  • Fulll aibu....Mfanyabiashara abambwa laivu gesti na mwanafunzi Mfanyabiashara ‘alwatani’ Bongo, mkazi wa jijini Dar, Allain Tajiri amekumbwa na skendo nzito baada ya kufumaniwa na mwanafunzi wa sekondari wa kidato cha pili mwenye umri wa miaka 16. Tukio hilo la kusikitisha lilit… Read More
  • Mke wa mtu sumu NI kweli mke wa mtu sumu! Lakini hata mume wa mtu naye sumu! Katika Gazeti la Uwazi ambalo ni ndugu damu mmoja na hili, toleo la 786, Aprili 16-22, 2013 ukurasa wa mbele kulikuwa na habari kubwa; MHESHIMIWA AUMBUKA! Ka… Read More
  • EXCLUSIVE: UWOYA, DIAMOND wanaswa hotelini! WALIKODI NA KULALA CHUMBA NAMBA 208 WALIINGIA USIKU WAKATOKA MCHANA KWEUPE AMA KWELI MAPENZI YA MASTAA NI MAJANGA Unaweza kukwepa matone ya mvua lakini siyo kamera za Global Publishers Ltd, zinapoamua kukufanyia kazi, … Read More

0 maoni: