Friday, 15 August 2014

Mkono wa rubani wang'oka hewani


Rubani mmoja nchini Uingereza alipoteza mwelekeo angani akiendesha ndege ya biria baada ya mkono wake wa bandia kuchomoka wakati alipokua akielekea kutua.
Rubani huyo wa shirika la ndege la Flybe mwenye umri wa miaka 46 , aliruka kutoka uwanja wa ndege wa Birmingham, akiwa na abiria wapatao 47 ndani yake, wakati alipokaribia kutua katika uwanja wa ndege wa mji wa Belfast alikumbana na upepo mkali angani ambao ulimsababisha atue kwa ghafla ilivyo bahati hakukuwa na madhara kwa ndege yenyewe wala abiria.

Katika maelezo aliyoyatoa baada ya manusura, mkurugenzi wa shirika hilo la ndege la Flybe Captain Ian Baston, anayehusika pia na masuala ya usalama katika shirika hilo la Flybe alimuelezea rubani kiongozi wa ndege hiyo aliyekua akiiongoza kuwa ni mwenye uzoefu wa hali ya juu na mwenye kuaminiwa pindi awapo angani, na hivyo usalama wa abiria na wahudumu huwa katika mikono iliyo salama sana .

Muda mfupi tu kabla ya kuielekeza ndege Dash 8 kutua kwa dharula rubani huyo alijikagua na kuona kwamba mkono wake bandia wa shoto ulikua sawa lakini baada ya tukio hilo ghafla akajikuta mkono huo umechomoka.

Ndege hiyo ilitua kwa mlio mkubwa ingawa hakuna mtu aliyejeruhiwa na pia ndege haikuharibika.

Rubani alisema atakuwa makini zaidi katika siku za usoni kuhusiana na mkono wake huo bandia.

Kwa hisani ya BBC Swahili

Related Posts:

  • SHARUWA atoa waosia kwa Mastaa wa Kibongo KWENU, Wasanii mnaong’aa katika sanaa mbalimbali nchini. Ninafurahi kuwasiliana nanyi tena kwa wakati mmoja baada ya kuachana muda mrefu uliopita. Naamini mpo sawa na michakato ya kusaka mkate wa kila siku inaendelea vy… Read More
  • Namfuata MWISHO Namibia LICHA ya Mwisho Mwampamba kuwa mume wa ndoa wa Meryl Shikwambane, msanii wa filamu na muziki Bongo, Baby Madaha amesema anajiandaa kwenda nchini Namibia wanapoishi wanandoa hao kwa lengo la kujumuika na Mwisho na kula ba… Read More
  • LADY JAYDEE Vs Clouds MWANAMUZIKI Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, juzi Jumatatu hatimaye yalimkuta baada ya kuibua simanzi nzito katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, Dar, alipofikishwa baada ya kufunguliwa kesi ya madai namba 29/2013 na mabos… Read More
  • LEMA abaka? BINTI mrembo aitwaye Flora Bahati Lyimo (pichani) anamtuhumu mbunge mmoja ‘mtata’ wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linaloongozwa na Spika Anne Makinda (jina tunalo) kuwa amembaka, Uwazi lina kisa cha aibu ya … Read More
  • Msanii wa ZE COMEDY afanya uchafu beach MSANII memba wa Kundi la Ze Comedy linaloruka kupitia Runinga ya East Africa, Master Face amenaswa akifanya uchafu wa kushikana ‘kimalovee’ na msanii mwenzake aitwaye Happy ambaye alikuwa ametinga kivazi cha nusu utupu. … Read More

0 maoni: