Saturday, 14 December 2013

Penzi la AFANDE SELE na MAMA TUNDA kwisha?

Picha ya familia: Kutoka kulia ni Asha Shiengo ‘Mama Tunda’, Selemani Msindi ‘Afande Sele’, Asantesana Selemani na Tunda Selemani.

KUCHA za Shetani zimeugusa uchumba wa muda mrefu kati ya msanii Selemani Msindi ‘Afande Sele’ na Asha Shiengo ‘Mama Tunda’  ambapo inadaiwa sasa kila mmoja yuko na ‘hamsini’ zake, Ijumaa linaibumburua. Kwa mujibu wa chanzo chetu, kutoelewana kwao kunachangiwa na kucheleweshwa kwa ndoa baina yao pamoja na mambo mengine ambayo hakuwa tayari kuyaanika. “Kwa kifupi mapenzi sasa hivi kati ya Afande na Mama Tunda ni ‘vululuvululu’, kila mmoja yuko kivyake.
“Chanzo kikubwa ni kucheleweshwa kwa ndoa ambapo Afande anaonekana kupotezea suala la kuoana ,” kilisema chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa  jina lake gazetini.

Mwandishi wetu alipomtafuta Afande Sele kuweka wazi juu ya tuhuma hizo, kwa sauti ya upole kabisa alikiri kutokuwepo maelewano baina yake na mzazi mwenziye huyo huku akishindwa kubainisha haswa chanzo cha kutengana kwao.
“Ni kweli, kwa sasa siko na Mama Tunda, mimi niko Morogoro na yeye yuko Dar,” alisema msanii huyo bila ufafanuzi wa ziada.

Hata hivyo Mama Tunda alipotafutwa kwa njia ya simu, alissema chanzo cha mambo yote ni kutovalishwa pete ya ndoa.

“Chanzo ni hicho tu, nimechoka kukaa kwenye uchumba kwa muda mrefu ni miaka 15 sasa, hadi Tunda amefikisha miaka 13, si ni ajabu hiyo na sasa tuna mtoto wa pili ambaye ana miaka 2 bado ni wachumba tu, nimechoka,” alisema Mama Tunda na kisha kukata simu.
Wawili hao wamejaliwa watoto wawili, Tunda Selemani (13) na Asantesana Selemani (2).

Kwa hisani ya GPL

Related Posts:

  • Haponi mtu IMEBAINIKA kwamba kuna mtandao wa askari ndani ya majeshi mbalimbali ya ulinzi nchini na hasa Jeshi la Magereza ambao unajihusisha na biashara ya madawa ya kulevya. Uchunguzi wa Uwazi umebaini kwamba tayari orodha ya… Read More
  • Mambo ya Chuma ulete yamtokea MREMBO puani.... MREMBO mmoja, Rukia Omari mkazi wa Mbezi Beach jijini Dar amebambwa akidaiwa kuiba fedha kwa njia za miujiza eneo la  Bunju Mwanjenje kwenye duka la Wapemba. Imeelezwa kuwa katika tukio hilo, Rukia alichukua fed… Read More
  • Ndoa yangu haivunjiki leo wala kesho..... Aunt EZEKIEL MWANADADA anayetamba katika filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel amefunguka kuwa ndoa yake haiwezi kuvunjika leo wala kesho kwani amejipanga kikamilifu. Aunt aliyasema hayo kwa madai kuwa watu wengi wamekuwa wak… Read More
  • Mfanyabiashara wa Kihindi adaiwa kumnyonga Mwalimu.... Simanzi, majonzi na masikitiko makubwa yalitawala katika msiba wa Mwalimu Elizabeth Mmbaga, 22, aliyekutwa amefariki dunia chumbani kwake Kimara Baruti jijini Dar, Aprili 15 mwaka huu, Uwazi lina mkanda mzima. Haba… Read More
  • Full Aibu NI aibu sana! Ndivyo unavyoweza kusema juu ya Oparesheni ya Fichua Maovu iliyosimamiwa na Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar, OCD Wilbroad Mutafungwa na Ofisa wa Oparesheni, Inspekta Jacob Swai kwa kushi… Read More

0 maoni: