Tuesday, 12 November 2013

Wanalipwa kwa kunyonyesha watoto Uingereza

Akina mama waliojifungua watoto nchini Uingereza wanalipwa hadi pauni miambili kuwanyonyesha watoto wao. Huu ni mradi mpya ulioanzishwa nchini Uingereza kwa usihirkiano kati ya serikali na watafiti wa utabibu, katika mitaa ya Yorkshire Kusini na Derbyshire, ili kuwahamaisha akina mama umuhimu wa kuwanyonyesha wanao wachanga.

Mradi huo pia unatarajiwa kufanywa katika eneo lengine la tatu katika mradi ambao utawalenga akina mama 130 watakaojifungua watoto kuanzia sasa hadi mwezi Machi mwaka ujao.
Ikiwa mradi huu utafanikiwa basi huenda ukafanyika kote nchini Uingerezea, mwaka ujao.
Mradi huu wa kutumia pesa kuwahamisha akina mama kunyonyesha watoto wao, sio mpya nchini Uingereza.
Umewahi kujaribiwa katika kuwahamisha wavutaji sigara kuacha tabia hiyo na watu wanene kupata lishe bora.
Lakini hii bila shaka ni mara ya kwanza kuwalipa akina mama kuweza kuwanyonyesha watoto wao.
Katika mradi huo, akina mama kutoka katika maeneo fulani ya Sheffield na Chesterfield watepewa vocha zenye thamani ya pauni miambili, ambazo wanaweza kutumia katika maduka makubwa na ya kifahari kununua bidhaa.
Maeneo hayo, yameteuliwa kwa utafiti huu kwa sababu akina mama hawawanyonyeshi kabisa watoto wao.
Imegunduliwa kuwa ni mama mmoja tu kati ya wanne anayenyonyesha hadi wiki ya sita ikilinganishwa na sehemu zengine nchini humo.
Ili kupata vocha hiyo, mama atalazimika kumnyonyesha mwanawe hadi miezi sita
Wakunga na maafisa wa afya watahitajika kuhakikisha kuwa wale wanaoshiriki kwenye mradi huo wanapata pauni miamoja na ishirini ikiwa watanyonyesha kwa wiki za kwanza sita.
Mradi huu umetokana na tofauti zilizopo za kiafya , utafiti ukionyesha kuwa kuwanyonyesha watoto kunasaidia kuzuia matatizo ya kiafya kwa watoto kama kuumwa na tumbo, maradhi ya kifua pamoja na kuwasaidia watoto kiakili.
Daktari Clare Relton, mmoja wa wataalamu wanaohusika na mradi huo amesema kuwa anatuami mradi huo utawasaidia wanawake kuona umuhimu wa kunyonyesha watoto wao.
Chanzo - BBC Swahili

Related Posts:

  • Tumsaidie Mtoto Hamisi tumuokoe kwenye mateso! Tafadhalini msaada wadau! Mtoto Hamis Hashim Bakari, mwenye umri wa miaka 13, anapata mateso makubwa akisumbuliwa na tatizo la miguu kujaa maji kutokana na kugundulika kuwa na mifupa laini tangu mwaka 2008.  Mtoto Ha… Read More
  • Breastfeeding Early breast milk is liquid gold – Known as liquid gold, colostrum (coh-LOSS-trum) is the thick yellow first breast milk that you make during pregnancy and just after birth. This milk is very rich in nutrients&nb… Read More
  • How to get pregnant fast: 12 top tips for getting pregnant Trying to get pregnant can be a lot of fun - you've always got an excuse to snuggle up with your partner and have some luvin'. But while lots of people think that getting pregnant will just take a matter of … Read More
  • 10 Best Detox Foods You Should Start Eating Detoxing has become bit of a trend with all the different fasting formulas and super foods that are out there. Unfortunately, most of the popular “detoxes” really aren’t safe for you and aren’t healthy either. If you want … Read More
  • Why is green tea so healthy? The magic ingredient is green tea, which is well known for its cancer-fighting properties. Natural antioxidants called polyphenols in the tea help block the growth of skin cancer cells. In fact, green tea has a whole … Read More

0 maoni: