Friday, 27 September 2013

Mambo usiyoyajua kuhusu super star wa Filamu wa Ghana aliyetua kwenye ardhi ya Kikwete VAN VICKER; ‘FROM ZIRO TO HERO’

Joseph Van Vicker (Nollywood actor)
AMEZALIWA maskini, ameishi kwenye umaskini, kukosa mahitaji muhimu, akakosa elimu na fursa mbalimbali za maendeleo lakini hatimaye kipaji cha kuigiza kinakuja kumtoa. Huyo ndiye Van Vicker (pichani kushoto). Staa huyo ambaye ana mvuto runingani, alikanyaga ardhi ya Jakaya Kikwete, Tanzania mwishoni mwa wiki iliyopita kwa shughuli za kikazi na Amani lilifanikiwa kufanya naye mahojiano:
KUZALIWA
Alizaliwa Agosti 1, 1977 nchini Ghana. Wazazi wake wana asili ya mataifa mawili tofauti. Baba yake ni raia wa Uholanzi, mama yake ni raia wa Ghana na Liberia. Staa huyo anasema alipozaliwa wazazi wake walimpa jina la Fhiphi. Neno hilo ni la Kighana, linamaanisha mtu aliyezaliwa Ijumaa. Jina la Van lililokuja baadaye pia ni neno la Kiholanzi ambalo maana yake ni ‘mtoto wa’.  Vicker lilikuwa ndiyo jina la baba yake hivyo Van Vicker maana yake ni mtoto wa Vicker. Hata hivyo baadaye mkali huyo alibatizwa kanisani na kupewa jina Joseph. Baba na mama wa staa huyo walikutana Liberia ambapo baba yake alikuwa akifanya kazi kwenye shirika moja la ugavi wa umeme nchini humo.
PIGO
Akiwa na umri wa miaka sita, Van Vicker alipata pigo la kuondokewa na baba yake.“Siwezi kuzungumzia sana suala hilo yule ni mzazi wangu japokuwa sikubahatika kupata malezi yake, toka hapo maisha kwangu yalikuwa magumu,” alisema Vicker.

ELIMU
Mkali huyo hakutaka kuzungumzia sana elimu yake, lakini aliweka bayana kuwa ana maarifa ya kutosha na zaidi hupenda kujielimisha mwenyewe juu ya mambo mbalimbali ya kila siku. “Elewa tu kwamba nilisoma katika ngazi ya kawaida, nilipata bahati ya kusoma shule ambayo aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan, alisoma. Inaitwa Mfantsipim,” alisema.
KABLA YA KUIGIZA
“Kabla sijaanza kuigiza, nilikuwa Mtangazaji wa Radio Groove 106.3 FM ya Ghana,” alisema Vicker na kuongeza: “Kabla sijaanza kutangaza, nilipitia msoto wa hali ya juu kwani wakati huo pia sikuwa na baba. Maisha yalikuwa magumu, kila mtu alinitenga, nilidharaulika sana, machozi yalikuwa sehemu ya maisha yangu.”

KUIGIZA RASMI
“Mwaka 1999 nilikutana na jamaa mmoja, akaniunganisha kwenye dili la filamu, nikacheza filamu kwanza iitwayo Devine Love, hapo ndipo maisha yalipoanza kuninyookea,” alisema.

MAPENZI VIPI?
“Sikuwahi kujihusisha sana na masuala ya mapenzi utotoni, kutokana na jinsi hali ya kutengwa. Nilianza kupigana na maisha baada ya kutoka shule,” alisema.  Mwigizaji huyo alizidi kutiririka kuwa, alikutana na mkewe Adjoa mwaka 1999 wakadumu kwenye uhusiano wa kimapenzi na kufanikiwa kufunga ndoa mwaka 2004.
WATOTO  
Van Vicker family pictures
Kwa sasa Van na mkewe wana watoto watatu, J’dyl, J-ian na Joseph Van Vicker II (pichani). Anasema hana mpango wa kuongeza watoto.

MICHEZO ANAYOIPENDA:
Mbali ya uigizaji, Vicker anapenda sana michezo kama mpira wa miguu, tennis na basketball.

Kuhusu mafanikio, mwigizaji huyo hakutaka kufunguka moja kwa moja utajiri wake lakini alidai kipato anachokipata kutokana na sanaa kinamwezesha kufurahia maisha yake.


TUZO
Vicker aliweka wazi kuwa amewahi kushinda tuzo mbalimbali lakini ambazo hawezi kuzisahau ni mbili za mwanzoni ambazo ni Ghana Awards Best Actor (Local Films) na Ghana Award Best Director (Leading Role).
BAADHI YA KAZI ZAKE:  
Vicker amefanya kazi nyingi sana za kuigiza, kwa harakaharaka alisema anakumbuka sinema kama mia moja, lakini anazozikubali zaidi ni Devine Love, In the Eyes of my Husband, River of Tears, Innocent Soul, American Boy na Beyonce: The President’s Daughter.

AMEJIFUNZA NINI TANZANIA?
“Kila mtu ni mpole, mkarimu, mcheshi hivyo vitu vikubwa ambavyo nimejifunza Tanzania,” alisema Vicker.


Habari kwa hisani ya GPl

Related Posts:

  • Daz Baba Kwishey MASKINI Daz Baba! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia habari ya kusikitisha ya msanii huyo ambaye jina lake kamili ni David Jacob kunaswa akiwa amezima mjini hapa huku ulevi wa kupindukia ukidaiwa kuwa chanzo. Daz Baba … Read More
  • RAY C anajuta kumjua LORD EYES........... Rehema Chalamila ‘Ray C’ akiwa na Lord Eyez enzi hizo. INAWEZEKANA umekuwa ukisikia vitu vingi kuhusu lejendari wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ lakini hukupata chansi ya kumsikia mwenyewe akifunguka mwanzo mwis… Read More
  • DIAMOND ampa mimba mtoto wa shule na kuingia mitini...... MREMBO aliyetimuliwa shule akiwa kidato cha nne baada ya kutundikwa mimba, Sasha Juma ameibuka na madai kuwa amezaa na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’. MCHEZO MZIMA - Habari kutoka kwa chanzo ch… Read More
  • Huu ndio Utajiri wa Marehemu Askofu KULOLA NI maswali tata yameibuka baada ya mazishi ya aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Evengelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Dk. Moses Samuel Kulola (85) kwamba, ameacha utajiri wa kiasi gani wakati wa uhai wake, Uwazi… Read More
  • Ndoa ya Mzee MAJUTO chali! MWANAMKE anayedaiwa kufunga ndoa ya siri na mchekeshaji mahiri Bongo, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto au King Majuto, Rahma Abdallah (20 - pichani), ameibuka na kudai kutelekezwa na mumewe huyo. Ndoa hiyo ambayo… Read More

0 maoni: