Friday, 27 September 2013

Mambo usiyoyajua kuhusu super star wa Filamu wa Ghana aliyetua kwenye ardhi ya Kikwete VAN VICKER; ‘FROM ZIRO TO HERO’

Joseph Van Vicker (Nollywood actor)
AMEZALIWA maskini, ameishi kwenye umaskini, kukosa mahitaji muhimu, akakosa elimu na fursa mbalimbali za maendeleo lakini hatimaye kipaji cha kuigiza kinakuja kumtoa. Huyo ndiye Van Vicker (pichani kushoto). Staa huyo ambaye ana mvuto runingani, alikanyaga ardhi ya Jakaya Kikwete, Tanzania mwishoni mwa wiki iliyopita kwa shughuli za kikazi na Amani lilifanikiwa kufanya naye mahojiano:
KUZALIWA
Alizaliwa Agosti 1, 1977 nchini Ghana. Wazazi wake wana asili ya mataifa mawili tofauti. Baba yake ni raia wa Uholanzi, mama yake ni raia wa Ghana na Liberia. Staa huyo anasema alipozaliwa wazazi wake walimpa jina la Fhiphi. Neno hilo ni la Kighana, linamaanisha mtu aliyezaliwa Ijumaa. Jina la Van lililokuja baadaye pia ni neno la Kiholanzi ambalo maana yake ni ‘mtoto wa’.  Vicker lilikuwa ndiyo jina la baba yake hivyo Van Vicker maana yake ni mtoto wa Vicker. Hata hivyo baadaye mkali huyo alibatizwa kanisani na kupewa jina Joseph. Baba na mama wa staa huyo walikutana Liberia ambapo baba yake alikuwa akifanya kazi kwenye shirika moja la ugavi wa umeme nchini humo.
PIGO
Akiwa na umri wa miaka sita, Van Vicker alipata pigo la kuondokewa na baba yake.“Siwezi kuzungumzia sana suala hilo yule ni mzazi wangu japokuwa sikubahatika kupata malezi yake, toka hapo maisha kwangu yalikuwa magumu,” alisema Vicker.

ELIMU
Mkali huyo hakutaka kuzungumzia sana elimu yake, lakini aliweka bayana kuwa ana maarifa ya kutosha na zaidi hupenda kujielimisha mwenyewe juu ya mambo mbalimbali ya kila siku. “Elewa tu kwamba nilisoma katika ngazi ya kawaida, nilipata bahati ya kusoma shule ambayo aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan, alisoma. Inaitwa Mfantsipim,” alisema.
KABLA YA KUIGIZA
“Kabla sijaanza kuigiza, nilikuwa Mtangazaji wa Radio Groove 106.3 FM ya Ghana,” alisema Vicker na kuongeza: “Kabla sijaanza kutangaza, nilipitia msoto wa hali ya juu kwani wakati huo pia sikuwa na baba. Maisha yalikuwa magumu, kila mtu alinitenga, nilidharaulika sana, machozi yalikuwa sehemu ya maisha yangu.”

KUIGIZA RASMI
“Mwaka 1999 nilikutana na jamaa mmoja, akaniunganisha kwenye dili la filamu, nikacheza filamu kwanza iitwayo Devine Love, hapo ndipo maisha yalipoanza kuninyookea,” alisema.

MAPENZI VIPI?
“Sikuwahi kujihusisha sana na masuala ya mapenzi utotoni, kutokana na jinsi hali ya kutengwa. Nilianza kupigana na maisha baada ya kutoka shule,” alisema.  Mwigizaji huyo alizidi kutiririka kuwa, alikutana na mkewe Adjoa mwaka 1999 wakadumu kwenye uhusiano wa kimapenzi na kufanikiwa kufunga ndoa mwaka 2004.
WATOTO  
Van Vicker family pictures
Kwa sasa Van na mkewe wana watoto watatu, J’dyl, J-ian na Joseph Van Vicker II (pichani). Anasema hana mpango wa kuongeza watoto.

MICHEZO ANAYOIPENDA:
Mbali ya uigizaji, Vicker anapenda sana michezo kama mpira wa miguu, tennis na basketball.

Kuhusu mafanikio, mwigizaji huyo hakutaka kufunguka moja kwa moja utajiri wake lakini alidai kipato anachokipata kutokana na sanaa kinamwezesha kufurahia maisha yake.


TUZO
Vicker aliweka wazi kuwa amewahi kushinda tuzo mbalimbali lakini ambazo hawezi kuzisahau ni mbili za mwanzoni ambazo ni Ghana Awards Best Actor (Local Films) na Ghana Award Best Director (Leading Role).
BAADHI YA KAZI ZAKE:  
Vicker amefanya kazi nyingi sana za kuigiza, kwa harakaharaka alisema anakumbuka sinema kama mia moja, lakini anazozikubali zaidi ni Devine Love, In the Eyes of my Husband, River of Tears, Innocent Soul, American Boy na Beyonce: The President’s Daughter.

AMEJIFUNZA NINI TANZANIA?
“Kila mtu ni mpole, mkarimu, mcheshi hivyo vitu vikubwa ambavyo nimejifunza Tanzania,” alisema Vicker.


Habari kwa hisani ya GPl

Related Posts:

  • Bongo kila siku mapya.... Baada ya Shilole Kupiga Mkwara Sinta aandika hivi .............. Seriously najisikia raha sana pale ninapotafutwa kama udi  na uvumba especially ninafanya nini na mambo yangu yananiendeleaje, kumbe nina kikiiii ya hatariii aaah sana, Thank u sweeriesss maana ninajisikia burudani w… Read More
  • Yanayojiri mujini............... Ally Kiba na Madam Rita? Habari za mujini sasa hivi ni Ally Kiba na Madam Rita............  mambo yalianza kutag na kulike, ila sasa kuna hatua nyingine.......... inasemekana sasa hivi Ally Kiba  anaendesha gari ya Madame........ na an… Read More
  • Kuna ukweli wowote katika hili? Ndugu zanguni, LEMA, ile kesi ya kubaka bado nasumbuliwa na polisi huku, Naomba uje usafishe jina lako please! Siku hizi nimekuwa mnyonge sana kwani polisi wa huku UK wamekuwa wakinipigia simu mara kwa mara wakitaka kuj… Read More
  • WEMA azua timbwili Wema Isaac Sepetu akiwa amefura kwa hasira. STAA wa filamu za Kibongo asiyekaukiwa vimbwanga, Wema Isaac Sepetu amezua bonge la timbwili kwa wafanyakazi wake wa ndani wa kiume na kike akiwemo mlinzi, Amani linakuletea kis… Read More
  • Shilole kaiba simu za Diamond? TAA wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ ameingia matatani akidaiwa kuingia mitini na simu tatu za mkononi alizoaminiwa nchini Afrika ya Kusini alikokwenda kufanya shoo.Msanii huyo alikumbwa na kas… Read More

0 maoni: