Wednesday, 20 February 2013

Ndoa hupangwa na MUNGU! Mama yake Monalisa (NATASHA) achumbiwa.....

LICHA ya kuwa mtu mzima mwenye mtoto na wajukuu wawili, staa wa filamu Bongo, Suzan Lewis ‘Natasha’ amechumbiwa. Habari za uhakika kutoka katika chanzo chetu makini zinasema kwamba, Natasha alivalishwa pete ya uchumba wikiendi iliyopita, Yombo – Dovya, Dar na mwanaume anayetambuliwa kwa jina Alex Humba Ludamila.

“Ilikuwa hafla ya siri kubwa, Natasha hakutaka kabisa waandishi wa habari na kwakweli siwezi kukutajia eneo lakini fahamu kwamba ni Yombo – Dovya. Unajua huyu ni mwanaume wake wa muda mrefu na walikuwa wakiishi pamoja lakini jamaa kaamua kuchukua jumla ndiyo maana amefuata taratibu zote,” kilieleza chanzo hicho.
Pekupeku za Tollywood Newz zilinasa kuwa, kwa sasa mipango ya ndoa imepamba moto na ndoa inatarajiwa kufungwa mapema mwezi Mei, mwaka huu. Juhudi za kumpata Natasha ili azungumzie suala hilo ziligonga mwamba baada ya simu yake kutopatikana muda wote Jumapili na juzi Jumatatu alipopigiwa.

Kwa hisani ya GLP

Related Posts:

  • !!!!!!!!!!!!!!!!!!????????????? Mke wa mtu huyo.......... Maadili yako wapi? hata kama ndio usupa star mmmmmmmmmmh hii imezidi!!  unapofikia kuitwa mume au mke wa mtu kuna baadhi ya vitu inabidi kuvipunguza na kama inawezekana kuviacha kabisa.................. … Read More
  • Kumbe Q Chillah nae kama Ray C? Wimbi la Wasanii wa Muziki wa kibongo kuingia kwenye matumizi ya madawa ya kulevya kumbe ni kubwa kuliko inavyojulikana na wengi, hivi karibuni wambea wa mjini tulizinyaka habari kuwa Msanii mahiri wa muziki wa B… Read More
  • Uozo wa Msanii Nora Waanikwa na Aliye Kuwa Mumewe MUME wa mcheza filamu mahiri za Kibongo Nuru Nassoro ‘Nora’, Masoud Ally ‘Luqman’ ameamua kuvunja ukimya baada mkewe huyo kueleza sababu zilizofanya ndoa yao kuvunjika ambazo anadai siyo za kweli. Akizungumza na mwand… Read More
  • KESI YA LULU YAHAMIA MAHAKAMA KUU Msanii wa filamu za maigizo nchini, Elizabeth Michael ‘Lulu’ leo amerudishwa rumande baada ya kusomewa kesi yake mpya ya kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba. Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu jijini Da… Read More
  • Habari njema !!!erikali Imechukua Jukumu la Kumtibu Sajuki Serikali imechukua jukumu la kumhudumia msanii na muongozaji wa filamu Sadick Juma Kilowolo ambaye anatarajia kuondoka wiki ijayo kuelekea India kwa matibabu. Katibu wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Wilson Maku… Read More

0 maoni: