People's Magazine
The place where you can find everything...
Home
Wednesday, 27 February 2013
Home
»
Celebrities News
» JOSEPH SHALUWA amchana live JACK wa CHUZ
JOSEPH SHALUWA amchana live JACK wa CHUZ
By
Unknown
14:05
No comments
Kwako,
Jacqueline Pentizel ‘Jack wa Chuz’. Pole kwa changamoto ulizokutana nazo juzi hotelini wakati ukiwa na mteja aliyetaka kuspendi na wewe kwa dola 500. Ni ajali kazini, usiwaze sana.
Tatizo nini ujue sister? Unawadanganya watu. Unapindisha ukweli kuwa uongo. Hapo ndipo ulipokosea zaidi. Siku zote binadamu anapokuwa mkweli ndipo anakuwa huru.
Kudanganya wakati mwingine kunaweza kuwa na maana kama unaongopa kwa lengo la kuficha kitu chenye manufaa lakini pia uwe na ushahidi au mazingira ambayo unaowadanganya hawatakushtukia.
Ni kweli wewe ni muongo, tena muongo mkubwa mwenye ‘shahada ya kwanza ya uongo’ uliyoipata katika Visiwa vya Madagascar ila sasa inaonekana huko ‘chuoni’ ama ulikuwa unachungulia majibu au ulikuwa unatoka na profesa akawa anakubeba!
Gazeti hili toleo lililopita liliripoti habari ya kukunasa ukiwa kwenye mtego wa kwenda kuuzwa kwa ajili ya kufanya ngono kwa dola 500. Siyo siri, muuazaji mwenyewe ni Baby Candy na anaujua ukweli huu, kuwa alikuwa kazini kukuuza. Ushahidi wa kutosha upo.
Kama chombo cha habari siku zote tuko macho kumulika maovu yanayofanywa kwenye jamii. Tukiwa katika kutimiza majukumu hayo hata siku moja hatumsingizii mtu. Tunasimama katika ukweli.
Tunajua ukweli unauma na wengi hawapendi kuambiwa ukweli, wewe ni kati ya watu hao. Mbaya zaidi wakati ukikanusha kwenye runinga unajua wazi kuwa tukio ni la kweli na si filamu kama ulivyokuwa ukijaribu kudanganya.
Nidhamu na maadili unapaswa kusimamia mwenyewe, ukiteleza na kunaswa usitumie nguvu kukanusha, kuwa mkweli. Yaani umenaswa ukitaka kuingia mzigoni na mapatano yamefanyika tena kila kitu kimerekodiwa, gazeti linatoka asubuhi jioni yake tayari upo kwenye kituo cha runinga unakanusha!
Hebu kuwa mkweli mtoto wa kike, kuna filamu ya aina ile? Wasomaji wa Global kwa namna walivyo makini na wakomavu hawawezi kukubaliana na upuuzi uliouongea kwenye runinga. Wanajua unatapatapa tu!
Eti unasema ulikuwa unarekodi filamu?! Ipi? Prodyuza ni nani na mhusika mkuu ni yupi sasa pale? Acha uongo wa kitoto. Ili usiandikwe ishi kwa staha. Wewe ni mtu maarufu, watu wanajifunza kupitia maisha yako, utawaponza hata wasanii wengine chipukizi wenye nia ya kuingia kwenye soko la filamu wazuiwe na wazazi wao wakiamini lipo soko jingine nyuma ya filamu.
Kuishi kwa kutegemea biashara haramu hakuna maana, umepewa kipaji cha sanaa, kwa nini usikitumie vizuri kutafuta riziki yako badala ya kutafuta shotikati?
Acha uongo wa kizamani. Nakuasa usitumie mwavuli wa sanaa kufanya mambo machafu yasiyokubalika katika jamii ya kistaarabu ya Kitanzania.
Utakuwa muungwana kama ukirudi tena kwenye jamii yako na kuitaka radhi si kukanusha kwa maelezo yasiyo na mbele wala nyuma. Fikisha salamu zangu kwa Baby Candy.
Yuleyule,
Mkweli daima,
Joseph Shaluwa
Kwa hisani ya GLP
Email This
BlogThis!
Share to X
Share to Facebook
Categories:
Celebrities News
← Newer Post
Older Post →
Home
0 maoni:
Post a Comment
Social Profiles
Popular
Tags
Blog Archives
Search this Blog
Heavy Metal Lover! Lady Gaga goes back to the Eighties with ripped high waisted glitter jeans and a sweet rock and roll tribute T-shirt to her father Joe
Heavy metal lover: Lady Gaga stepped out in an Eighties rock inspired ensemble in New York on Thursday
Male tansgender prisoner guilty of brutal murder is moved from women's jail 'because he kept having sex with female inmates' while waiting for sex-change op funded by UK taxpayer
Paris Green, 22, allowed to stay in women's prison ahead of sex-change op He has now been moved amid suspicions of liaisons with other...
Unaleta usanii jumba la sanaa?
Mandelas at war: Winnie fires first salvo, saying leader’s daughter from his first marriage should be head of the family and not rival grandson Mandla
Winnie Madikizela-Mandela has said oldest living child should head family Makaziwe Mandela is Nelson's only surviving child from his f...
Rihanna getting traditional Polynesian tattoo by Inia Taylor & assisted ...
Inside El Salvador's secretive prison pits where notorious gangs are crammed together like livestock in cells the size of a shed
New report reveals the shocking conditions that members of El Salvador's violent and bloody MS-13 and M18 gangs are forced to live in ...
Grammy Awards ya mwaka huu hatari tupu... hebu angalia vizazi vilivyobamba
RAY C anunua gari?
Sinta na Mange wana bifu? Soma hapa chini
Sinta Mange
Hatimaje Mama LULU na Mama KANUMBA waenda BUKOBA kula kiapo cha Undugu
Kutoka kushoto: Flora Mtegoa, Lulu na Lucresia Karugila katika pozi. ULE udugu wa ukubwani kati ya wazazi wa mastaa wa filamu Bongo, ...
Powered by
Blogger
.
My favorite News blog
Loading...
Celebrities Gossip
Loading...
.
Tags
Afya
(116)
Broken heart stories
(1)
Celebrities kids
(18)
Celebrities News
(783)
Children
(4)
Death Anouncement
(1)
Dini
(27)
Elimu
(5)
Extraordinary People
(12)
Familia
(26)
Full aibu
(87)
General
(20)
Karibu Jamvini
(1)
Katuni
(11)
Kazi za Jamii
(3)
Magazeti pendwa
(228)
Mahusiano
(281)
Majanga
(16)
mambo ya kuiga
(3)
Mapishi
(2)
Michezo na Burudani
(49)
Mikasa ya Maisha
(2)
Mila na desturi
(14)
Moyo Mpweke
(3)
Msaada kwenye tuta...
(10)
Nyumba
(28)
OMG
(476)
OMG... Black are beautiful
(10)
Picha huongea
(25)
Sayanzi na Tekinolojia
(3)
Siasa
(82)
Tangazo
(2)
Tiba Mbadala
(4)
True story
(77)
Ugaidi
(1)
Ukatili
(55)
umaarufu kazi
(28)
Urembo
(20)
Video
(10)
Vipaji
(3)
Vituko mtaani
(164)
Vivazi na Mitindo
(171)
Wanaume
(32)
Wanawake
(121)
0 maoni:
Post a Comment