Monday 11 November 2013

Msanii wa bongo Flava afumwa live Makaburini na mchumba wa mtu.....

MREMBO aliyetajwa kwa jina moja la Ema aliyedai kuwa ni mchumba wa jamaa aliyemtaja kwa jina la Amri au Mdudu amefumaniwa laivu akisaliti penzi na mwanaume mwingine. Tukio hilo la aina yake lilijiri kwenye Makaburi ya Buguruni, Dar, mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kuwekewa mtego.
TAARIFA KWA OFM

Wakati makachero wa Oparesheni Fichua Maovu wakiwa kwenye ‘patroo’ walipokea taarifa kutoka kwa chanzo chake ambacho kiliomba wafike katika makaburi hayo ambapo kulikuwa na fumanizi.
OFM: Fumanizi la aina gani? Isije ikawa ni wanandoa tukaingia chaka.

Chanzo: Hawa bado ni wachumba tu. Jamaa alikuwa anamfuatilia mchumba’ke amemnasa na jamaa kwenye gari wakifanya mapenzi sasa kuna timbwili zito.

OFM: Una uhakika na unachokisema?
Chanzo: Kama hamtaki acheni (akakata simu).

OFM KAZINI

Kwa kuwa OFM haipuuzii habari, ilimteua ‘kamanda’ wake mmoja ambaye aliwasha bodaboda na kuwahi eneo la tukio.
Huku sekeseke likiendelea makaburini hapo, Mdudu ambaye alikuwa na jazba ya kuibiwa ‘mali’ zake alisema kuwa alitonywa na rafiki zake kwamba mchumba’ke huyo yupo katika Baa ya Kimboka, Buguruni akijirusha na jamaa huyo.

Mdudu alisema aliamua kwenda katika baa hiyo na kubana sehemu huku akishuhudia kila kitu. 

“Unajua nimekuwa nikiambiwa tu kuwa Ema ananisaliti lakini nilikuwa napuuzia.
“Sasa nimeamini baada ya kumshuhudia mwenyewe akisaliti penzi letu,” alisema Mdudu.

VIKAO VYA HARUSI

Alisema kuwa Ema ni mchumba’ke na anaishi na wazazi wake Buguruni-Malapa, Dar na ameshamtolea mahari.
“Ndiyo tumeanza kupanga vikao vya harusi vifanyike katika Baa ya Wazee iliyopo Ilala-Amana (Dar),” alisema.

Alisema baada ya kuwasubiri hadi usiku wa manane, aliwaona wakiinuka na kuingia kwenye teksi ndipo na washikaji zake nao wakachukua bodaboda na kuifuata ile teksi kwa nyuma bila wahusika kushtuka.
WAKUTWA LAIVU

Alisema walishangaa kuona gari lile likipaki maeneo ya Makaburi ya Buguruni kisha dereva akatoka na kwenda kusimama mbali kidogo akivuta sigara.
“Machale yakanicheza nikawatonya wanangu kuwa tusubiri kama dakika kumi halafu tukaivamie teksi.

“Baadaye uzalendo ulinishinda ikabidi nikavamie. Ndipo tukawakuta laivu wanavua nguo wakiwa kimahaba,” alisema Mdudu.

Alisema roho ilimuuma alipomkuta mchumba’ke huyo ambaye anampenda kwa dhati akiwa katika hali ile, nusura apoteze fahamu na mara baada ya kuwavamia waliwatoa nje ndipo sekeseke likaanza.

KUMBE NI MSANII! 

Wakati mtiti ukiendelea, yule mwanaume mwingine aligundulika kuwa kumbe ni msanii wa Bongo Fleva aliyejitambulisha kwa jina la Spince Seseme.

Akihojiwa na Ijumaa Wikienda kulikoni kufumaniwa na mke wa mtu, Spince alisema hakufahamu kama Ema ni mchumba wa mtu kwani kama angefahamu asingetoka naye kimapenzi.
ANATUMIA UMAARUFU WAKE?

Jamaa huyo aliyeimba Wimbo wa Ayaya akimshirikisha Ali Kiba alidai alifahamiana na Ema siku nyingi na hawakuwahi kuvunja amri ya sita.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wanaomjua jamaa huyo, eti amekuwa akitumia umaarufu wake kupindua uhusiano wa watu na kuapa kumkomesha.

“Kama polisi wakishindwa tutamwendea kwa babu ili ajue cha mtu mali,” alisikika brazameni mmoja.

POLISI

Hata hivyo, tukio hilo lilimalizika kwa kila mmoja kukimbilia Kituo cha Polisi cha Buguruni akidai kupigwa ambapo hadi OFM inaondoka walikuwa wakichukuliwa maelezo.


Angalia picha zaidi za tukio hapa chini
Mchumba wa mtu akipewa kichapo baada ya kufumaniwa.

Watuhumiwa baada ya kutolewa kwenye teksi walimokuwa wanafanya yao.

...Mchumba wa mtu akizidi kupokea kipondo.

Mchumba wa mtu akitoka nduki baada ya kuchoropoka mikononi mwa jamaa waliokuwa wakimpa kipigo.

Kwa hisani ya GPL

0 maoni: