Tuesday 15 January 2013

Kimenuka Scorpion Girls yaanza kusambaratika.......Jack Chuzi Ndani

Kundi la Muziki la wadada wa Mjini Machachari la Scorpion girls lililovuma kwa kasi mwishoni mwa mwaka jana limetangaza kumpiga chini member mmoja wa kundi hilo anayejulikana kwa Jina la Rashida Wanjara kwa kile kinachodaiwa kuwa hayupo serious na kazi.....Msemaji wa kundi hilo Bella amesema wameamua kumrudisha member wa kundi hilo wa zamani anayejulikana kwa Jina la Jack Chuzi.... Kundi hilo kwa sasa linaundwa na Bella, Mariam Jolwa aka Jini Kabula na Jack Chuzi

0 maoni: