Tuesday 30 April 2013

Kanuni 12 za kukufanya uwe na ndoa yenye furaha na mafanikio.

NDOA inaweza kufananishwa kama safari ndefu yenye matukio yasiyotazamiwa, yenye milima na mabonde, yenye mazuri na mbaya, mengine yenye kupendeza na mengine yenye kuumiza. Hali zisizotazamiwa zinaweza kutokeza vizuizi visivyotarajiwa, vingine vikionekana kuwa vikubwa sana. Hata hivyo, watu wengi humaliza safari hiyo kwa furaha na mafanikio, wakiwa wamekabili matatizo madogo tu. Kwa kweli, mafanikio katika ndoa hayapimwi kwa panda shuka za safari bali yanapimwa kwa jinsi wenzi wanavyoshughulikia hali hizo. jaribu kuangalia kanuni muhimu ambazo zinaweza kukuongoza katika safari ya ndoa yenye furaha na mafanikio.

1. Ione ndoa kuwa takatifu-usiione ndoa kama kitu cha kawaida kama urafiki wa kawaida tu.

2. Zungumza kwa heshima-busara na heshima mbele siku zote epuka kuropoka hovyo.

3. Sitawisha fadhili kwa mwezi wako-kama hana mpe,mkiwa navyo nyote peaneni.

4. Onesha huruma kwa lolote lile linalojitokeza kama changamoto kwa mwezi 
wako.
5. Onyesha unyenyekevu-Pande zote me/ke onyesheni unyenyekevu

6. Usiudhike haraka-Punguza uharaka wa hasira hata kama kuna maudhi.

7. Jua wakati wa kukaa kimya-tulia jibu baada ya kutafakari.

8. Onyesha hisia kwa mwenzio unaposikiliza lolote kutoka kwake.
9. Uwe na zoea la kuonyesha uthamini-mthamini mwenzio kwa vitendo

10. Uwe mwenye haraka kusamehe-Usiweke vitu moyoni.

11. Uwe mwaminifu kwa mwenzi wako na kwa ndoa yako-heshimu amri za mwenyenzi MUNGU

12. Imarisheni ushikamanifu-mshikamane katika hali zote.

0 maoni: