Monday 21 January 2013

Baby wangu anapenda kudeka ! wenye wivu kwa kweli wajinyonge ...


STAA wa filamu Bongo, Tamrina Poshi ‘Amanda’(pichani) amefunguka kuwa kipenzi chake, Emmannuel Rushau ‘Bwana Misosi’ anapenda kudeka pindi wanapokuwa viwanja.

Akiongea  kwa mbwembwe namwandishi wetu katika Viwanja vya Leaders Club hivi karibuni, Amanda aliweka wazi kuwa mpenzi wake huyo amekuwa na tabia hiyo hali ambayo inaleta maswali mengi kwa wasiolipenda penzi lao.

“Jamani Baby wangu naye anadeka... hebu tazama sasa hivi alivyonilalia, majungu yataanza sasa hivi. Lakini nilikuwa nikiomba faraja, sasa nimeipata nashukuru,”alisema Amanda.


Kwa hisani ya GLP

0 maoni: