Sunday 20 January 2013

Jamani WAMAMA jihadharini na KIM .....

Bi. Mwele Malechela,

Najua utashangaa sana kuusoma huu ujumbe. Usishangae mshukuru Mungu kwa kuzipata taarifa hizi. Nimeona njia nzuri kukupatia ni kukueleza ukweli kwa njia hii kuhusu mtu unayejihusisha naye sasa hivi anayejiita Kim. Majina yake halisi ni Kimbangambanga Julius Mgaya. Jamaa ni mtu mbaya na hatari sana. Wewe ni mtu mwenye heshima mbele ya jamii na mkubwa sana kiumri kujihusisha kimapenzi na Kim. Waswahili wanasema mapenzi hayachagui ni sawa isipokuwa tabia mbaya za mtu huyo ndio tatizo. Jamaa ameshatapeli sana hapa mjini na kuwarubuni wanawake wengi wenye nafasi zao kimapenzi na mwisho wa siku anawatapeli na kuwachuna mali zao.

Kim anafahamika sana hapa mjini kwa kuishi maisha ya kitapeli, utasikia hadithi nyingi kuwa yupo bize ana mikutano hadi usiku na wafanyabiashara au viongozi wa serikali kumbe ni uongo, hiyo ni kutaka kujionyesha kwa watu kuwa ni mtu muhimu na wa maana. Safari nyingi anazofanya ndani na nje ya nchi ni za kitapeli. Ana wanawake anaowachuna wapo Marekani na UK. Maisha yake yote ni utapeli na kupitia wanawake wenye nyadhifa au wafanyabiashara wakubwa. Kinachomsaidia ni utanashati wake wanawake humnunulia vitu vya thamani. Kim amesoma hadi kidato cha nne tu hana cheti chochote zaidi ya hapo. Kim anajifanya ni mbia kwenye biashara kubwa kubwa hapa mjini akijichanganya na wahindi na viongozi wakubwa. Ukweli ni kwamba hana kitu na yeye ni kishoka tu anawahangaikia watu mahali walipokwama na yeye analipwa kamisheni yake. Anatangaza mjini kuwa majengo yaliyobomolewa kule Masaki ni yakwake, kumbe ni ya mfanyabiashara mwenye asili ya kihindi. Anasema anamiliki hoteli Arusha inayoitwa Snowcrest, ukweli ni kwamba hoteli hiyo inamilikiwa na kijana wa kichaga anayeitwa Willy pamoja na dada yake anayeitwa Theo. Kujihusisha kwa Kim kwenye hoteli hiyo ni kwa ajili ya kutafuta biashara na uurafiki wake na mmiliki wa hoteli hiyo lakini amekuwa anajifanya ni mali yake.

Mama yangu Mwele, nakueleza mambo ya Kim ili usiingie kwenye mtego wake. Anakuhadaa ili mbadilishane magari, usithubutu. Kwa muda sasa amekuwa akikushawishi umpe gari lako nayeye akupe gari lake aina ya Benz . Benz hilo alikuwa amelipaki muda mrefu bila kulitembeza, sio la kwake. Benz lina kesi maana alimdhurumu mwanamke mmoja na sasa mwenyewe amechachamaa analitaka gari lake. Sasa kuziba kasheshe hilo anataka kukuingiza wewe mkenge ili yeye ajitoe. Mama chukua tahadhali bado mapema. Kim anapenda sana kubadilisha magari lakini yasikubabaishe, yote unayoyaona sio mali yake ni ya kutaperi na kubadilishana na watu kama anavyotaka kukufanyia. Alishawahi kuwa na gari aina ya Hammer lakini halikuwa la kwake, alimtapeli mwanamke Zanzibar mwenyewe husema kwa watu kuwa ameliuza. Alichukua magari mawili kwa Chikawe yule waziri wa sheria mojawapo ni BMW X5 ya rangi ya kibluu hadi leo hajamrudishia na anajizungusha nayo.

Chikawe anamuonea aibu kumdai kwa kuwa alimsaidia kumtafutia nyumba binti yake. Kim alivyo sasa hivi ana mahusiano ya kimapenzi na binti huyo wa Chikawe anayeitwa Tamika ameolewa na mzungu lakini utafikiri Kim ndio mume wake alivyomganda. Kim alikuwa na magari mengine Suzuki Grand na Mitsubishi ambazo si mali yake. Magari hayo kabla ya kunyang’anywa na mwenye mali alimtapeli mama mmoja anayefanya kazi shirika la nyumba NHC, ofisi yake ipo Msasani. Mama huyo mtu mzima aliingizwa mkenge na Kim baada ya kuingia kwenye uhusiano wa kimapenzi. Na kwa kuwa mama huyo anafanya kazi NHC alimsaidia Kim kuipata nyumba ya nationa house anayoishi sasa Kim Chang’ombe. Nyumba hiyo aliipata kitapeli kwa msaada wa huyo mama, wakaibomoa na kujenga nyumba nyingine kubwa ambayo ndio anaishi Kim sasa hivi. Huyo mama aliyafanya yote hayo akijua kuwa wataishi na Kim kama mume na mke. Nyumba ilipoisha Kim hakumjali tena huyo mama jambo lililomfanya mama wa watu ajue kuwa ametaperiwa na kumyang’anya magari yake mawili Suzuki Grand na Mitsubishi. Hivi sasa mama wa watu yupo mbioni kuikomboa nyumba hiyo ya Chang’ombe maana kaijenga kwa jasho lake. Kuna gari nyingine tena saloon Progress ambayo nayo haikuwa yakwake. Gari hiyo alimtapeli dada mmoja anayeitwa Lucy ambaye ameolewa na Mkorea wanamiliki kampuni inayoitwa TAKAOKA. Kama kawaida yake Kim alianzisha uhusiano wa kimapenzi na dada huyo huku akimshawishi wafungue kampuni. Lucy alimpa pesa nyingi Kim, gari na jenereta kubwa lilifungwa kwenye nyumba ya Kim huko Chang’ombe. Lucy alipomshtukia Kim akachachamaa na kumnyang’anya gari na jenereta, hataki hata kumsikia Kim. Mama Mwele ona mifano ya wenzio.

Tabia nyinginewe ya Kim ni umalaya. Kila mwanamke anataka kulala naye, wengi anawaahidi kuwaoa na hata kuwavisha pete. Anatumia mbinu hiyo chafu ili kuwanasa nyie dada zetu akishapata anachokitaka anatafuta pengine pa kuchuna. Kuna mwanamke aliyezaa naye Zanzibar, baada ya kukorofishana aliondoka na mtoto wake. Sasa hivi amezaa mtoto wa kiume na mwanamke mwingine polisi traffic anayeitwa Shufaa anakaa Ukonga. Mwanamke mwingine yupo benki ya NBC, kuna mwingine naye anaishi Kibangu ni vurugu tupu. Kuna wanawake wawili ambao ana mahusiano nao bila wao kujijua wanafanya kazi Ifakara health institute. Mmoja wao anaitwa Rahima Dosa ambaye naye kama walivyo wengine amemtolea posa baada ya mdosi kuona Kim anamzingua. Rahima ameapiza kuwa hawezi kumuacha Kim vinginevyo atamuua kwa kua ameshampotezea muda wake mwingi. Wakati huo huo ana mahusiano ya kimapenzi na wanawake wengi nitakutajia wachache ninaowafahamu na ambao Kim ameshanitambulisha nao akina Premi Kibanga yupo ikulu ni mwanamke wake wa muda mrefu, Sofia, Badra Masud wa Tanesco, Justina Shauri, Shina Sanare, Batilda Buriani balozi wa Kenya ambaye alikuwa mbunge zamani, Grace, Mange Kimambi na mama yake Rose Kimambi ambao wote amelala nao na wengineo. Arusha pia ana wanawake wawili ninaowafahamu mmoja nafanya kazi kwenye hoteli moja maarufu na mwingine anafanya kazi BOT Arusha.

Kwanini nimesukumwa kukujulisha tabia za Kim, pamoja na udhaifu wetu wanaume ni kitendo kibaya kuwachanganya wanawake wanaofahamiana au ndugu. Sijuwi mlikutana wapi na Kim lakini kabla hujaanza kuwa karibu naye aliwahi kuwa na mahusiano na dada mmoja ambaye sitakutajia ni wa familia yenu alianzisha uhusiano naye wa kimapenzi akamwambia anataka kumuoa, dada huyo akapata mimba. Kim akamwambia aitoe mimba dada huyo akakataa kuitoa. Kim kwa siri alitafuta dawa na kumpa binti atumie akimdanganya kuwa ni za vitamin zisaidie kukuza mimba hiyo. Dada huyo kwa mapenzi alitumia dawa hizo na akaanza kuumwa tumbo na damu kumtoka, alipoenda hospitali aliulizwa ametumia nini naye akaonyesha dawa alizopewa na Kim kumbe hakupaswa kuzitumia kabisa katika ujauzito na mimba ilitoka. Dada huyo si mbali na familia yako lakini jamaa haoni vibaya anachotaka ni kuvuna. Huyo si mwanaume mama achana naye atakuliza. Kibaya zaidi tabia ya umalaya haogopi hata magonjwa wala hajifunzi maana mfano mzuri ni watu wake wa karibu ambao ni wazazi wake walitangulia mbele za haki kutokana na ugonjwa wa ukimwi lakini yeye hajali.

Sasa hivi kuna watu wanajiandaa kumfungulia mashitaka ya utapeli na kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu. Amewaliza wengi na watu wanavisasi naye. Kwa kupenda maisha ya juu ametengeneza maadui kuliko marafiki na amekuwa anaishi maisha ya kujifichaficha. Kim hana mwisho mzuri. Jihadhari sana na Kim anapenda sana ushirikina na waganga wa kienyeji. Anatumia waganga wengi kutoka Bagamoyo, Zanzibar na Iringa. Na utapeli wake ni wa kutumia dawa kuwafunga watu wanaomdai na kuwapumbaza wenye pesa zao ili wasimshtukie. Mwaka jana mwanzoni kuna taarifa zake zilitoka kwenye vyombo vya habari na magazetini zikitahadharisha watu kukaa mbali na Kim. Habari hizo zilitumwa kwenye vyombo vyote vya habari pamoja na picha yake. Habari hizo naziunganisha hapa chini ili usome kama hukubahatika kuzisoma mwaka jana. Ningeweza kukueleza mengi kuhusu Kim ni aibu kwa haya machache huenda ikasaidia kukufungua macho. Jamii inakuheshimu sana na ndicho
kilichoniumiza na nikaamini humjuwi vizuri Kim.

Mdau 

0 maoni: