People's Magazine
The place where you can find everything...
Home
Wednesday, 27 February 2013
Home
»
Celebrities News
» JOSEPH SHALUWA amchana live JACK wa CHUZ
JOSEPH SHALUWA amchana live JACK wa CHUZ
By
Unknown
14:05
No comments
Kwako,
Jacqueline Pentizel ‘Jack wa Chuz’. Pole kwa changamoto ulizokutana nazo juzi hotelini wakati ukiwa na mteja aliyetaka kuspendi na wewe kwa dola 500. Ni ajali kazini, usiwaze sana.
Tatizo nini ujue sister? Unawadanganya watu. Unapindisha ukweli kuwa uongo. Hapo ndipo ulipokosea zaidi. Siku zote binadamu anapokuwa mkweli ndipo anakuwa huru.
Kudanganya wakati mwingine kunaweza kuwa na maana kama unaongopa kwa lengo la kuficha kitu chenye manufaa lakini pia uwe na ushahidi au mazingira ambayo unaowadanganya hawatakushtukia.
Ni kweli wewe ni muongo, tena muongo mkubwa mwenye ‘shahada ya kwanza ya uongo’ uliyoipata katika Visiwa vya Madagascar ila sasa inaonekana huko ‘chuoni’ ama ulikuwa unachungulia majibu au ulikuwa unatoka na profesa akawa anakubeba!
Gazeti hili toleo lililopita liliripoti habari ya kukunasa ukiwa kwenye mtego wa kwenda kuuzwa kwa ajili ya kufanya ngono kwa dola 500. Siyo siri, muuazaji mwenyewe ni Baby Candy na anaujua ukweli huu, kuwa alikuwa kazini kukuuza. Ushahidi wa kutosha upo.
Kama chombo cha habari siku zote tuko macho kumulika maovu yanayofanywa kwenye jamii. Tukiwa katika kutimiza majukumu hayo hata siku moja hatumsingizii mtu. Tunasimama katika ukweli.
Tunajua ukweli unauma na wengi hawapendi kuambiwa ukweli, wewe ni kati ya watu hao. Mbaya zaidi wakati ukikanusha kwenye runinga unajua wazi kuwa tukio ni la kweli na si filamu kama ulivyokuwa ukijaribu kudanganya.
Nidhamu na maadili unapaswa kusimamia mwenyewe, ukiteleza na kunaswa usitumie nguvu kukanusha, kuwa mkweli. Yaani umenaswa ukitaka kuingia mzigoni na mapatano yamefanyika tena kila kitu kimerekodiwa, gazeti linatoka asubuhi jioni yake tayari upo kwenye kituo cha runinga unakanusha!
Hebu kuwa mkweli mtoto wa kike, kuna filamu ya aina ile? Wasomaji wa Global kwa namna walivyo makini na wakomavu hawawezi kukubaliana na upuuzi uliouongea kwenye runinga. Wanajua unatapatapa tu!
Eti unasema ulikuwa unarekodi filamu?! Ipi? Prodyuza ni nani na mhusika mkuu ni yupi sasa pale? Acha uongo wa kitoto. Ili usiandikwe ishi kwa staha. Wewe ni mtu maarufu, watu wanajifunza kupitia maisha yako, utawaponza hata wasanii wengine chipukizi wenye nia ya kuingia kwenye soko la filamu wazuiwe na wazazi wao wakiamini lipo soko jingine nyuma ya filamu.
Kuishi kwa kutegemea biashara haramu hakuna maana, umepewa kipaji cha sanaa, kwa nini usikitumie vizuri kutafuta riziki yako badala ya kutafuta shotikati?
Acha uongo wa kizamani. Nakuasa usitumie mwavuli wa sanaa kufanya mambo machafu yasiyokubalika katika jamii ya kistaarabu ya Kitanzania.
Utakuwa muungwana kama ukirudi tena kwenye jamii yako na kuitaka radhi si kukanusha kwa maelezo yasiyo na mbele wala nyuma. Fikisha salamu zangu kwa Baby Candy.
Yuleyule,
Mkweli daima,
Joseph Shaluwa
Kwa hisani ya GLP
Email This
BlogThis!
Share to X
Share to Facebook
Categories:
Celebrities News
← Newer Post
Older Post →
Home
View mobile version
0 maoni:
Post a Comment
Social Profiles
Popular
Tags
Blog Archives
Search this Blog
Magazeti pendwa
!!!!!!!!????????????
!!!!!!!!!
Forbes 40 Most Powerful Celebrities In Africa
According to Forbes, several of your favorite icons that were previously featured on Golden Icons were mentioned as part of “The 40 Most P...
The woman who has endured 416 hours of pain covering her body in tattoos... that she'll never see because she's BLIND
Fran Atkinson has spent last three years having colourful ‘body suit’ inked But because of an eye condition she has no idea what her artwo...
Why Men Cheat On Good Women?
According to the good people at Bossip , here’s 9 reasons why men cheat on good women. Men/Women…do you agree? Now I will say this, wome...
JIDE: Mimi na GARDNER tunaishi kama kaka na dada!
Kumbe! Super woman katika Afro-Pop, Judith Wambura a.k.a Lady Jaydeee au Jide amefunguka kuwa yeye na mumewe, Gardner Habash ‘Kapteini’ ...
Ethiopia's Karo people decorate their faces and bodies with chalk and ochre to boost chances of finding love - and scare off rivals
The Karo tribe use red ochre and white chalk to create intricate designs on their faces and bodies Both sexes do it as a way to be more v...
Idris arudi na midola Tanzania ..... angalia matukio muhimu ya safari yake
Ilianza hivi........ Ni nani atabeba hili begi la chuma? Memory Wall Presentation Enjoyment Things Never been fr...
Makahaba watumia ARV'S badala ya Kondomu
Cheza katika media player Madaktari nchini Kenya wameelezea wasiwasi kuhusu matumizi mabaya na ya kiholea ya dawa za dharur...
Powered by
Blogger
.
My favorite News blog
Loading...
Celebrities Gossip
Loading...
.
Tags
Afya
(116)
Broken heart stories
(1)
Celebrities kids
(18)
Celebrities News
(783)
Children
(4)
Death Anouncement
(1)
Dini
(27)
Elimu
(5)
Extraordinary People
(12)
Familia
(26)
Full aibu
(87)
General
(20)
Karibu Jamvini
(1)
Katuni
(11)
Kazi za Jamii
(3)
Magazeti pendwa
(228)
Mahusiano
(281)
Majanga
(16)
mambo ya kuiga
(3)
Mapishi
(2)
Michezo na Burudani
(49)
Mikasa ya Maisha
(2)
Mila na desturi
(14)
Moyo Mpweke
(3)
Msaada kwenye tuta...
(10)
Nyumba
(28)
OMG
(476)
OMG... Black are beautiful
(10)
Picha huongea
(25)
Sayanzi na Tekinolojia
(3)
Siasa
(82)
Tangazo
(2)
Tiba Mbadala
(4)
True story
(77)
Ugaidi
(1)
Ukatili
(55)
umaarufu kazi
(28)
Urembo
(20)
Video
(10)
Vipaji
(3)
Vituko mtaani
(164)
Vivazi na Mitindo
(171)
Wanaume
(32)
Wanawake
(121)
0 maoni:
Post a Comment